Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Hakimu Anaweza Kurekebishwa?

Je, Hakimu Anaweza Kurekebishwa?

Je, Hakimu Anaweza Kurekebishwa?

SLADJANA, ambaye ni Shahidi wa Yehova huko Croatia, alitakiwa afike mahakamani kwa ajili ya kesi iliyohusu masuala ya kifedha. Alifika mahakamani kwa wakati. Hata hivyo, mhusika mwingine katika kesi hiyo alichelewa. Sladjana alikuwa na hamu ya kutoa ushahidi, hivyo wote walipokuwa wakingojea, alijipa ujasiri na kuzungumza na hakimu.

“Bwana, je, ulijua kwamba hivi karibuni hakutakuwako mahakimu wala mahakama yoyote duniani?” akauliza. Kwa wazi, alikuwa akizungumza kuhusu mahakimu wa leo.

Kwa mshangao, hakimu alimtazama tu bila kusema lolote. Kisha kesi ikaanza. Ilipomalizika na Sladjana aliposimama ili kutia sahihi hati fulani, hakimu aliinama na kumnong’onezea hivi: “Je, una hakika kuhusu jambo ambalo umetoka tu kuniambia, kwamba hakutakuwa na mahakimu wala mahakama yoyote duniani?”

“Ndiyo, Bwana. Nina hakika kabisa!” akajibu Sladjana.

“Una uthibitisho gani wa jambo hilo?” hakimu akauliza.

“Uthibitisho unaweza kupatikana katika Biblia,” Sladjana akajibu.

Hakimu akasema angependa kusoma uthibitisho huo, lakini hana Biblia. Hivyo, Sladjana akaahidi kumletea Biblia. Mashahidi walimtembelea hakimu huyo, wakampa Biblia, na kumhimiza awe na funzo la Biblia la kila juma. Hakimu huyo alikubali kujifunza na muda si muda akawa Shahidi wa Yehova.

Unabii wa Zaburi 2:10 unasema hivi: “Na sasa, enyi wafalme, onyesheni ufahamu; kubalini kurekebishwa, enyi waamuzi [au mahakimu] wa dunia.” Inatia moyo kama nini watu kama hao wanapokubali kwa unyenyekevu kufuata mwelekezo wenye upendo wa Yehova!

[Picha katika ukurasa wa 32]

Sladjana akiwa na hakimu huyo