Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Tunapaswa Kuogopa Kuja Kwa Kristo?

Je, Tunapaswa Kuogopa Kuja Kwa Kristo?

Je, Tunapaswa Kuogopa Kuja Kwa Kristo?

UNA maoni gani kuhusu kuja kwa Yesu Kristo? Je, unaona kuja kwake kuwa tukio ambalo litaleta uharibifu, ukiwa, na adhabu kwa wanadamu? Au je, unatarajia kwamba kuja kwa Kristo kutakomesha matatizo yetu yote? Je, kuja kwake ni tukio ambalo tunapaswa kuogopa? Au je, tunapaswa kulitazamia kwa hamu?

Biblia inasema hivi kuhusu kuja kwa Kristo: “Tazama! Anakuja na mawingu, na kila jicho litamwona, . . . na makabila yote ya dunia yatajipiga-piga kwa huzuni kwa sababu yake.” (Ufunuo 1:7) Kuja huko kunahusu kuonekana kwa Yesu wakati ujao ili kuwathawabisha wenye haki na kuwaadhibu waovu.

Badala ya kuogopa tukio hilo, mtume Yohana alitazamia kwa hamu kuja kwa Kristo. Baada ya kupokea ufunuo kuhusu kuja huko na matokeo yake kuelekea dunia, Yohana alisali hivi kwa bidii: “Njoo, Bwana Yesu.” (Ufunuo 22:20) Lakini kwa nini ‘makabila yote ya dunia yanajipiga-piga kwa huzuni kwa sababu yake’? Ni katika maana gani “kila jicho” litamwona? Kuja kwa Kristo kutatimiza nini? Kuamini kuja kwake kunaweza kutufaidi jinsi gani sasa? Habari inayofuata itajibu maswali hayo.