Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umefurahia kusoma matoleo ya hivi karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ona kama unaweza kujibu maswali yafuatayo:

• Tunaweza kujifunza nini kutokana na mfano wa Yesu kuhusu mkaribishaji aliyeomba bila kuacha? (Luka 11:5-10)

Mfano huo unakazia mtazamo tunaopaswa kuwa nao tunaposali. Tunapaswa kuomba bila kuacha, au kuendelea kuomba, hasa ili tupewe roho takatifu ya Mungu. (Luka 11:11-13)—12/15, ukurasa wa 20-22.

• Mfano wa Yesu kuhusu mjane na mwamuzi unatufundisha nini? (Luka 18:1-8)

Unakazia uhitaji wa kusali. Tofauti na mwamuzi huyo, Yehova ni mwadilifu naye anataka kutusaidia. Zaidi ya hilo, tunapaswa kuwa na imani kama ya mjane katika mfano huo.—12/15, ukurasa wa 26-28.

• Kwa nini mtume Paulo aliwaambia Wakristo Wakorintho ‘wapanuke’? (2 Wakorintho 6:11-13)

Inaonekana kwamba watu fulani huko Korintho hawakuwathamini waamini wenzao. Hawakupanuka na hawakuwa na moyo wa ukarimu. Tunahitaji kujitahidi kusitawisha uthamini wa kweli kuelekea waamini wenzetu, hata kujitahidi kupata marafiki wapya.—1/1, ukurasa wa 9-11.

• Ni nini maana ya kutiwa muhuri kunakotajwa katika Ufunuo 7:3?

Mungu anapowatia mafuta Wakristo kwa roho takatifu, wanatiwa muhuri kwa mara ya kwanza. Lakini andiko la Ufunuo 7:3 linahusu kutiwa muhuri kwa mara ya mwisho, wakati inapothibitishwa kwamba watiwa-mafuta hao wameonyesha ushikamanifu wao kikamili.—1/1, ukurasa wa 30-31.

• Wazazi wanaweza kujifunza nini kutokana na simulizi la Biblia kumhusu Samweli?

Kwanza, wanapaswa kuwafundisha watoto wao neno la Mungu, kama wazazi wa Samweli walivyomfundisha. Kwa kuongezea, wanapaswa kuwatia moyo watoto wao wamtumikie Yehova maishani.—1/15, ukurasa wa 16.

• Tunaweza kuonyesha jinsi gani kwamba tunafurahia kumngojea Yehova?

‘Tunangojea siku ya Yehova,’ tukitazamia kupata kitulizo wakati atakapowaangamiza watu wote wasiomwogopa Mungu. (2 Petro 3:7, 12) Hata ingawa Yehova anatamani kukomesha uovu wote, anajizuia ili awaokoe Wakristo kwa njia ambayo itatukuza jina lake. Tunapaswa kuwa na hakika kwamba Yehova anajua wakati unaofaa wa kuchukua hatua, na kwa wakati uliopo tunapaswa kumsifu Mungu kwa bidii. (Zaburi 71:14, 15)—3/1, ukurasa wa 17-18.

• Je, Noa aliingiza ndani ya safina wanyama saba kati ya kila mnyama safi au vikundi saba vya wanyama wawili wawili?

Noa aliambiwa ‘ajichukulie saba saba’ kati ya kila mnyama aliye safi. (Mwanzo 7:1, 2) Katika Kiebrania, neno linalotumiwa linamaanisha kihalisi “saba saba.” Kurudia-rudia neno hilo hakumaanishi kwamba ni pea saba, kama maandiko mengine ya Biblia yanavyoonyesha. Kwa wazi, Noa alichukua wanyama saba kati ya kila mnyama, yaani, pea tatu, na mnyama wa saba ambaye angemtoa baadaye kuwa dhabihu. (Mwanzo 8:20)—3/15, ukurasa wa 31.

• Kwa nini Wakristo wanapaswa ‘kutafakari,’ jinsi imani ya wazee, ambao wanaongoza, inavyokuwa?

Mtume Paulo anatuomba ‘tutafakari,’ au tuangalie kwa makini, matokeo ya mwenendo wa uaminifu wa wazee na kuiga mifano kama hiyo ya imani. (Waebrania 13:7) Tunafanya hivyo kwa sababu tunaagizwa tufanye hivyo katika Neno la Mungu. Pia, tunasadiki kwamba wazee wanahangaikia kikweli mambo ya Ufalme na hali yetu njema.—4/1, ukurasa wa 28.