Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mlemavu Lakini Ana Tamaa ya Kutumika

Mlemavu Lakini Ana Tamaa ya Kutumika

Mlemavu Lakini Ana Tamaa ya Kutumika

UNAPOKUTANA kwa mara ya kwanza na Leonardo, huenda usifikiri kwamba anaweza kusaidia katika kazi ya ujenzi. Hana viganja vya mikono kwa sababu vilikatika katika msiba fulani kazini. Hata hivyo, ingawa Leonardo ni mlemavu, alikuwa akifanya kazi kwa bidii katika ujenzi huko Acajutla, El Salvador, kama unavyoweza kuona katika picha.

Ili ashiriki katika mradi wa ujenzi, Leonardo alijitengenezea vifaa vyake vya kazi. Kwa kawaida, anaingiza mkono wake wa kulia katika chuma kilichounganishwa na sepetu, yaani, kifaa cha kuchotea mchanga. Anatumia kifaa hicho kwa ustadi kujaza udongo katika kigari kidogo. Ameunganisha mikono ya kigari hicho na vyuma vya mviringo ili aweze kukisukuma. Ni nini kilichomchochea kushiriki katika mradi huo wa ujenzi?

Leonardo alitaka kushiriki katika ujenzi wa Jumba la Ufalme, au mahali pa ibada pa kutaniko la Mashahidi wa Yehova la kwao. Angetoa visingizio vingi ili kutoshiriki katika ujenzi huo. Alikuwa ameajiriwa kazi, alikuwa mlemavu, na alikuwa akitumika katika kutaniko lao akiwa mtumishi wa huduma. Hata hivyo, alitaka kumtumikia Mungu kadiri alivyoweza katika ujenzi huo pia.

Je, una roho kama hiyo katika kumtumikia Mungu? Badala ya kujitetea kwamba ni mlemavu, Leonardo alitumia akili yake kujitengenezea vifaa ili aweze kufanya kazi ambayo hangeweza kufanya. Alikuwa akimtumikia Mungu ‘kwa akili yake yote.’ (Mathayo 22:37) Iwe ni walemavu au si walemavu, watu wanaoshiriki katika ujenzi wa Majumba ya Ufalme ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote wana roho ya kujitolea. Watu wote wanaweza kuhudhuria mikutano yao, wewe pia unakaribishwa.