Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Ni Muhimu Zaidi Kuliko Hali ya Hewa

Ni Muhimu Zaidi Kuliko Hali ya Hewa

Ni Muhimu Zaidi Kuliko Hali ya Hewa

KARIBU mataifa yote yana methali kuhusu hali ya hewa. Mabaharia wanafurahi wanapoona anga jekundu wakati wa usiku. Wanajihadhari wanapoona anga jekundu asubuhi. Wataalamu wa hali ya hewa wanatoa sababu za kitaalamu zinazofanya hali ya hewa iwe kama msemo huo unavyoonyesha.

Katika siku za Yesu pia, watu walikuwa na desturi ya kuchunguza anga na kueleza jinsi ambavyo hali ya hewa ingekuwa. Yesu aliwaambia hivi Wayahudi fulani: “Inapokuwa jioni ninyi huwa na desturi ya kusema, ‘Kutakuwa na hali nzuri ya hewa, kwa maana anga ni jekundu’; na asubuhi, ‘Kutakuwa na baridi kali, na mvua leo, kwa maana anga ni jekundu, na lenye mawingu mazito.’ Mnajua jinsi ya kufasiri kuonekana kwa anga, lakini . . . “ Lakini nini? Yesu akaendelea kusema: “Ishara za nyakati hamwezi kuzifasiri.”—Mathayo 16:2, 3.

Hizo “ishara za nyakati “zilikuwa nini? Kulikuwa na mambo mengi yaliyoonyesha waziwazi kwamba Yesu alikuwa Masihi wa kweli aliyetumwa na Mungu. Matendo yake yalitambuliwa kwa urahisi kama tu anga jekundu. Hata hivyo, Wayahudi wengi walipuuza ishara zilizoonyesha kwamba Masihi alikuwa amekuja—jambo ambalo bila shaka lilikuwa muhimu zaidi kuliko hali ya hewa.

Leo pia, kuna ishara ambayo ni muhimu zaidi watu waelewe kuliko rangi ya anga. Yesu alitabiri kwamba ulimwengu huu mbovu utaharibiwa ili kuwe na ulimwengu bora zaidi. Alitaja mambo mbalimbali ambayo yakiwa pamoja yangeonyesha kwamba badiliko hilo limekaribia. Mambo hayo yanatia ndani vita ulimwenguni pote na njaa kali. Yesu alisema kwamba mambo hayo yakionekana, wakati wa Mungu wa kuingilia kati utakuwa umekaribia.—Mathayo 24:3-21.

Je, “unaona ishara za nyakati”?