Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Shahidi Mwaminifu Angani”

“Shahidi Mwaminifu Angani”

“Shahidi Mwaminifu Angani”

KWA muda mrefu watungaji wa mashairi na wa nyimbo wameusifu mwezi kuwa maridadi sana. Kwa mfano, wimbo mmoja ulioongozwa na Mungu unamtaja mwanamke ambaye ni “mrembo kama mwezi mpevu.” (Wimbo wa Sulemani 6:10) Naye mtunga-zaburi fulani anasema kishairi kwamba mwezi ni “shahidi mwaminifu angani.” (Zaburi 89:37) Maneno hayo kuhusu mwezi yanamaanisha nini?

Mwezi unamaliza kuizunguka dunia baada ya kila siku 27.3 bila kukosa. Hivyo, mwezi unaweza kusemwa kuwa mwaminifu kwa sababu unategemeka. Hata hivyo, huenda mtunga-zaburi huyo alikuwa akifikiria maana nyingine ya ndani. Aliuita mwezi “shahidi mwaminifu” katika wimbo wa kinabii uliohusu Ufalme ambao Yesu aliwafundisha wafuasi wake kusali juu yake.—Mathayo 6:9, 10.

Zaidi ya miaka 3,000 iliyopita, Yehova Mungu alifanya agano la Ufalme pamoja na Mfalme Daudi wa Israeli la kale. (2 Samweli 7:12-16) Kusudi la agano hilo lilikuwa kuandaa msingi wa kisheria wa Yesu Kristo kuketi kwenye kiti cha Ufalme milele akiwa mrithi wa Daudi. (Isaya 9:7; Luka 1:32, 33) Mtunga-zaburi aliimba hivi kuhusu kiti cha Ufalme cha “uzao” wa Daudi: “Kama mwezi, kitafanywa imara mpaka wakati usio na kipimo, na kama vile shahidi mwaminifu angani.”—Zaburi 89:36, 37.

‘Mwanga unaotawala usiku,’ yaani, mwezi, ni kikumbusho kinachofaa cha kudumu kwa utawala wa Kristo. Andiko la Danieli 7:14 linasema hivi kuhusu Ufalme wake: “Utawala wake ni utawala unaodumu mpaka wakati usio na kipimo ambao hautapitilia mbali, na ufalme wake ni ufalme ambao hautaharibiwa.” Mwezi ni shahidi ambaye anatukumbusha kuhusu Ufalme huo na baraka ambazo utawaletea wanadamu.

[Picha katika ukurasa wa 32 zimeandaliwa na]

Moon: NASA photo