Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Jina la Mungu Katika Muziki wa Kirusi

Jina la Mungu Katika Muziki wa Kirusi

Jina la Mungu Katika Muziki wa Kirusi

MWAKA wa 1877, mtungaji wa muziki anayejulikana sana, Modest Mussorgsky kutoka Urusi alichapisha kitabu cha nyimbo kinachotegemea jambo lililotukia katika nchi zinazotajwa katika Biblia. Alimwandikia hivi rafiki mmoja: “Nimetunga hadithi ya Kibiblia inayoitwa Jesus Navinus [Joshua], ambayo inategemea kabisa Biblia na hata inafuata njia zilizotumiwa na msafara wa ushindi wa Navinus katika Kanaani.” Katika nyimbo nyingine alizotunga, kutia ndani wimbo wa “Kuharibiwa kwa Senakeribu,” Mussorgsky alitumia pia masimulizi na watu wanaotajwa katika Biblia.

Katika hadithi ya “Jesus Navinus,” na vilevile katika chapa ya 1874 ya hadithi ya “Kuharibiwa kwa Senakeribu,” Mussorgsky anamtaja Mungu akitumia matamshi ya Kirusi ya jina la Mungu, ambayo yanawakilishwa katika Maandiko ya Kiebrania na konsonanti nne—יהוה (YHWH)—na konsonanti hizo zinaonekana karibu mara 7,000 katika Maandiko hayo.

Kwa hiyo, nyimbo hizo za Mussorgsky zinaonyesha kwamba kabla ya mwanzo wa karne ya 20, watu wa Urusi walijua vizuri sana jina la Mungu, Yehova, linalotajwa katika Biblia. Hilo ni jambo linalofaa kwa kuwa Yehova mwenyewe alimwambia Musa hivi: “Hilo ndilo jina langu mpaka wakati usio na kipimo, na huo ndio ukumbusho wangu kwa kizazi baada ya kizazi.”—Kutoka 3:15.

[Picha katika ukurasa wa 32]

Sheet music: The Scientific Music Library of the Saint-Petersburg State Conservatory named after N.A. Rimsky-Korsakov; street scene: National Library of Russia, St. Petersburg

[Picha katika ukurasa wa 32]

Hifadhi ya St. Petersburg mnamo 1913, mahali ambapo nakala zilizochapwa za muziki wa Mussorgsky zimehifadhiwa