Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kwa Nini Mungu Anaruhusu Uovu?

Kwa Nini Mungu Anaruhusu Uovu?

Kwa Nini Mungu Anaruhusu Uovu?

POPOTE unapotazama unaweza kuona uovu na mateso mengi. Raia na askari-jeshi wanauawa vitani. Jeuri na uhalifu umeenea sana. Labda umetendewa isivyo haki au kubaguliwa hivi karibuni. Inaelekea kwamba mambo hayo ambayo umeona na kutendewa yamekufanya uulize, ‘Kwa nini Mungu anaruhusu uovu?’

Hilo si swali jipya. Miaka 3,600 hivi iliyopita, Ayubu, mtumishi mshikamanifu wa Mungu aliuliza: “Kwa nini waovu wanaendelea kuishi?” (Ayubu 21:7) Akiwa amefadhaishwa na matendo maovu ya wananchi wenzake, nabii Yeremia aliyeishi katika karne ya saba K.W.K., aliuliza hivi: “Kwa nini njia ya waovu ndiyo imefanikiwa, kwamba wale wote wanaofanya hila ndio hawana wasiwasi?” (Yeremia 12:1) Ayubu na Yeremia walijua kwamba Mungu ni mwadilifu. Hata hivyo, walijiuliza kwa nini uovu ulikuwa mwingi sana. Labda wewe pia unajiuliza hivyo.

Watu fulani wanamlaumu Mungu kwa sababu ya uovu na mateso. Wengine wanauliza hivi: ‘Ikiwa Mungu ni mwenye nguvu zote, ana hekima na upendo, kwa nini hakomeshi uovu na mateso? Kwa nini ameruhusu uovu uendelee mpaka leo?’ Habari inayofuata inajibu maswali hayo na maswali mengine ya maana.

[Picha katika ukurasa wa 3]

AP Photo/Adam Butler