Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Kweli Ni Nini?”

“Kweli Ni Nini?”

“Kweli Ni Nini?”

YESU aliulizwa swali hilo kwa dharau na Gavana Mroma Pontio Pilato. Hakutaka ajibiwe, naye Yesu hakumjibu. Labda Pilato aliona kwamba haiwezekani kabisa kuielewa kweli.—Yohana 18:38.

Vivyo hivyo leo, watu wengi kutia ndani viongozi wa kidini, walimu, na wanasiasa, wanaidharau kweli. Wanaamini kwamba hakuna kweli kamili na kwamba kweli inabadilika sikuzote, hasa kweli kuhusu maadili na mambo ya kiroho. Bila shaka, hilo linamaanisha kwamba watu wanaweza kujiamulia wenyewe mambo yaliyo sawa na yaliyo makosa. (Isaya 5:20, 21) Pia, linawapa watu uhuru wa kukataa kanuni na viwango vya maadili ambavyo vilifuatwa na vizazi vya zamani na ambavyo wanaona kuwa vimepitwa na wakati.

Maneno yaliyomchochea Pilato kuuliza swali hilo yalikuwa muhimu sana. Yesu alisema hivi: “Kwa ajili ya hili mimi nimezaliwa, na kwa ajili ya hili nimekuja ulimwenguni, ili nitoe ushahidi juu ya ile kweli.” (Yohana 18:37) Yesu hakuamini kwamba kweli haieleweki na haiko wazi. Aliwaahidi wanafunzi wake hivi: “Mtaijua kweli, nayo kweli itawaweka ninyi huru.”—Yohana 8:32.

Lakini tunaweza kuipata wapi kweli hiyo? Pindi moja, Yesu alisema hivi alipokuwa akisali kwa Mungu: “Neno lako ni kweli.” (Yohana 17:17) Biblia, ambayo iliandikwa chini ya uongozi wa roho ya Mungu, inafunua kweli ambayo inatoa mwongozo na tumaini hakika kwa ajili ya wakati ujao, yaani, uzima wa milele.—2 Timotheo 3:15-17.

Pilato, alipuuza na kukataa nafasi ya kujifunza kweli hiyo. Namna gani wewe? Kwa nini usiwaulize Mashahidi wa Yehova “ile kweli” ambayo Yesu alifundisha ni nini? Watafurahi kukufundisha kweli hiyo.