Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Nilivutiwa na Azimio Lake Lenye Kustaajabisha”

“Nilivutiwa na Azimio Lake Lenye Kustaajabisha”

“Nilivutiwa na Azimio Lake Lenye Kustaajabisha”

GÜNTER GRASS, mtungaji wa vitabu Mjerumani na mshindi wa Tuzo la Nobeli la Vitabu mwaka wa 1999, alichapisha simulizi la maisha yake mnamo 2006. Katika simulizi hilo, anaeleza wakati alipoandikishwa katika kikosi cha ulinzi cha Ujerumani. Pia, katika simulizi hilo anaeleza kumhusu mtu ambaye alimvutia sana hivi kwamba angali anamkumbuka baada ya miaka zaidi ya 60 kupita. Mtu huyo alishikamana na imani yake chini ya mateso.

Katika mahojiano yaliyochapishwa katika gazeti fulani la kila siku (Frankfurter Allgemeine Zeitung), Grass anamkumbuka mtu huyo wa kustaajabisha, ambaye alikataa kuchukua silaha. Grass alisema kwamba mtu huyo “hakuunga mkono siasa za wakati huo, hakuwa Mnazi, Mkomunisti, wala Msoshalisti. Alikuwa Shahidi wa Yehova.” Grass hakumbuki jina la Shahidi huyo ambaye alimbandika jina la utani Hatufanyi-mambo-kama-hayo. Wachunguzi wa Mashahidi wa Yehova wanasema Shahidi huyo ni Joachim Alfermann. Alipigwa tena na tena na kuvunjiwa heshima, kisha akawekwa katika kifungo cha upweke. Lakini Alfermann aliendelea kuwa imara na akakataa kuchukua silaha.

“Nilivutiwa na azimio lake lenye kustaajabisha,” Grass akasema. “Nilijiuliza: Anaweza kuvumilia jinsi gani mambo yote hayo? Anakabiliana nayo kwa njia gani?” Baada ya kuvumilia jitihada nyingi za kuvunja utimilifu wake kwa Mungu, mwishowe Alfermann alipelekwa kwenye kambi ya mateso ya Stutthof mnamo Februari (Mwezi wa 2) 1944. Aliwekwa huru mnamo Aprili 1945, akaokoka vita, naye akaendelea kuwa Shahidi mshikamanifu wa Yehova mpaka alipokufa mwaka wa 1998.

Alfermann alikuwa mmoja wa Mashahidi 13,400 walioteswa kwa sababu ya imani yao nchini Ujerumani na pia katika nchi nyingine zilizomilikiwa na Wanazi. Walifuata mwelekezo wa Biblia wa kutounga mkono siasa na wakakataa kuchukua silaha. (Mathayo 26:52; Yohana 18:36) Mashahidi 4,200 hivi walifungwa katika kambi za mateso, na 1,490 wakapoteza maisha yao. Hata leo, msimamo waliochukua unawapendeza watu wengi ambao si Mashahidi wa Yehova lakini wanaovutiwa na uthabiti wao.

[Picha katika ukurasa wa 32]

Joachim Alfermann