Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umefurahia kusoma matoleo ya hivi karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ona kama unaweza kujibu maswali yafuatayo:

• Kwa nini “Agano la Kale” lina faida ya kudumu?

Mtungaji wake si mungu mkatili bali ni Mungu mwenye upendo, Yehova. Yesu na wafuasi wake wa mapema waliendelea kurejelea Maandiko ya Kiebrania. Yana mashauri yanayofaa kuhusu maisha ya kila siku na yanatoa tumaini zuri ajabu la wakati ujao.—9/1, ukurasa wa 4-7.

• Kuruhusu wakati upite tangu Adamu na Hawa walipoasi kumethibitisha nini?

Katika miaka 6,000 hivi ambayo imepita, Shetani amethibitishwa kuwa mwongo, kwa kuwa Adamu na Hawa na mamilioni ya wazao wao wamekufa. Kupita kwa wakati kumeonyesha kwamba wanadamu hawawezi kuwa na maisha mazuri bila kumtegemea Mungu na kwamba hawana haki wala uwezo wa kuongoza hatua zao.—9/15, ukurasa wa 6-7.

• Kwa nini Yakobo hakulaumiwa kwa sababu ya kujifanya kuwa Esau?

Yakobo alikuwa na haki ya kupokea baraka za baba yake kwa sababu alikuwa amenunua haki ya mzaliwa wa kwanza kutoka kwa Esau. Alipotambua kwamba alikuwa amembariki Yakobo, Isaka hakujaribu kubadili jambo hilo. Na ni wazi kwamba Mungu, ambaye ndiye angeingilia kati jambo hilo, alitaka Yakobo apokee baraka hizo.—10/1, ukurasa wa 31.

• Dhamiri yetu inaonyesha namna gani kwamba hatukutokana na mageuzi?

Katika kila jamii na utamaduni, watu wana mwelekeo wa kuwasaidia wengine, hata wanahatarisha maisha yao ili kufanya hivyo. Wanadamu hawangetazamiwa kuwa na mwelekeo wa kuwajali wengine bila uchoyo ikiwa wangekuwa wanyama tu ambao wanafanya kila wawezalo ili kuwa hai.—10/15, ukurasa wa 20.

• Kwa nini tuseme kwamba Mungu ni mnyenyekevu, anaonyeshaje sifa hiyo?

Akiwa Mwenye Enzi Kuu na Muumba, Mungu hana mipaka kama sisi. Hata hivyo, kulingana na 2 Samweli 22:36, Mungu ni mnyenyekevu katika maana ya kwamba anawajali na kuwahurumia wanadamu wa hali ya chini wanaojitahidi kumpendeza. Ni kana kwamba Mungu anajishusha ili ashughulike kwa fadhili na wale wanaomwogopa.—11/1, ukurasa wa 4-5.

• Vigae vya kale vinaunga mkono jinsi gani masimulizi ya Biblia?

Wachimbuaji wa vitu vya kale wamepata vigae huko Samaria vyenye majina saba ya ukoo yaliyoandikwa katika Yoshua 17:1-6. Vigae vya Aradi vinaunga mkono habari kuhusu familia za makuhani kutia ndani jina la Mungu. Vigae vya Lakishi vinafunua hali ya kisiasa na msukosuko uliokuwepo Yuda kabla ya mashambulizi ya Wababiloni.—11/15, ukurasa wa 12-14.

• Kwa nini tunakata kauli kwamba Luka ndiye aliyeandika kitabu cha Matendo?

Injili ya Luka na kitabu cha Matendo ya Mitume vimeelekezwa kwa Theofilo, na hilo linaonyesha kwamba vitabu hivyo viwili viliandikwa na Luka. Luka anatumia maneno yanayoonyesha kwamba alihusika katika matukio hayo. (Matendo 16:8-15)—11/15, ukurasa wa 18.

• Mkristo anapaswa kuwa na maoni gani kuhusu kuwinda na kuvua?

Tangu siku za Noa, Mungu aliwaruhusu wanadamu waue na kula wanyama. Hata hivyo, takwa la kumwaga damu yao linakazia kwamba uhai wa wanyama unapaswa kuheshimiwa kwa kuwa umetoka kwa Mungu. Wakristo hawapaswi kucheza michezo ya kuua wanyama au kuua ili kujifurahisha. Ni muhimu kutii sheria za Kaisari na kufikiria dhamiri za wengine. (Waroma 14:13)—12/1, ukurasa wa 31.