Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Suluhisho la Hekima

Suluhisho la Hekima

Suluhisho la Hekima

VIJANA watatu huko Afrika ya Kati walitaka kuhudhuria kusanyiko la wilaya katika eneo lao. Wangefanya nini ili wafike huko? Kusanyiko hilo lilifanyika umbali wa kilomita 90 hivi, na barabara zilikuwa mbaya na zenye vumbi, na hawakuwa na nauli. Waliamua kuazima baiskeli tatu lakini hawakupata baiskeli nzuri kwa ajili ya safari yao.

Mzee mmoja katika kutaniko lao alitambua tatizo lao, naye akawapa baiskeli yake iliyozeeka lakini inayofanya kazi. Aliwaeleza jinsi yeye na wengine walivyofanya zamani ili kufika kwenye kusanyiko. Mzee huyo aliwashauri wote watatu watumie baiskeli hiyo. Hilo lilikuwa suluhisho rahisi, lakini lenye kutatanisha. Watu watatu wangesafiri jinsi gani kwa baiskeli moja?

Ili kuepuka jua kali, ndugu hao vijana walikutana mapema asubuhi na kupakia mizigo yao kwenye baiskeli. Mmoja wao alitangulia kwa baiskeli, na wale wengine wawili walimfuata kwa miguu. Baada ya kuendesha baiskeli kwa mita 500, yule ndugu wa kwanza alisimama na kuegemeza baiskeli hiyo yenye mizigo kwenye mti. Bila shaka, alihakikisha kwamba ameiacha mahali ambapo wenzake wangeiona lakini ambapo haingeibwa na wapita-njia. Kisha aliendelea kutembea.

Wale wawili walipofika mahali ambapo baiskeli iliachwa, mmoja wao aliichukua na kuiendesha, na yule mwingine aliendelea kutembea kwa mita 500 kabla ya zamu yake. Hivyo, kwa kupanga mambo vizuri na kwa kuazimia, ndugu hao watatu walipunguza safari ya miguu kutoka kilomita 90 mpaka kilomita 60 hivi. Jitihada hizo hazikuwa za bure. Walikutana na ndugu na dada zao Wakristo kwenye kusanyiko hilo, nao wakafurahia karamu ya kiroho. (Kum. 31:12) Mwaka huu, je, utafanya yote unayoweza ili kuhudhuria kusanyiko la wilaya katika eneo lenu?