Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Yaliyomo

Yaliyomo

Yaliyomo

Agosti 15, 2008

Toleo la Funzo

MAKALA ZA FUNZO ZA MAJUMA YA:

Septemba (Mwezi wa 9) 29–Oktoba (Mwezi wa 10) 5

Yehova Hatawaacha Washikamanifu Wake

UKURASA WA 3

NYIMBO ZA KUTUMIWA: 114, 223

Oktoba 6-12

Dumisha Ushikamanifu Ukiwa na Moyo Kamili

UKURASA WA 7

NYIMBO ZA KUTUMIWA: 38, 8

Oktoba 13-19

Mheshimu Yehova kwa Kuonyesha Heshima

UKURASA WA 12

NYIMBO ZA KUTUMIWA: 48, 136

Oktoba 20-26

Yehova Anawatunza kwa Upendo Watumishi Wake Waliozeeka

UKURASA WA 17

NYIMBO ZA KUTUMIWA: 58, 216

Oktoba 27–Novemba (Mwezi wa 11) 2

Je, Unazungumza Ile “Lugha Safi” kwa Ufasaha?

UKURASA WA 21

NYIMBO ZA KUTUMIWA: 78, 169

Kusudi la Makala za Funzo

Makala ya Funzo ya 1 na ya 2 UKURASA 3-11

Makala hizi zinazungumzia jinsi Israeli lilivyogawanyika na kuwa ufalme wa kaskazini na wa kusini na kuonyesha kwamba Yehova hawaachi washikamanifu wake. Zinakazia kwamba tunahitaji kusitawisha sasa ushikamanifu kutoka moyoni ili kushinda vishawishi vya kupenda vitu vya kimwili au kimbelembele.

Makala ya Funzo ya 3 UKURASA 12-16

Makala hii inaonyesha kwamba kuuthamini utukufu wa Mungu kunaweza kuwa na uvutano mzuri juu yetu. Inachunguza yale ambayo tunaweza kujifunza kuhusu kuwaheshimu watu kutokana na jinsi Yesu alivyowatendea wengine. Jifunze pia jinsi tunavyoweza kuonyesha heshima.

Makala ya Funzo ya 4 UKURASA 17-21

Jifunze kuwaona Wakristo waliozeeka kama Yehova anavyowaona. Ona jinsi Biblia inavyotusaidia kuheshimu ujuzi na uzoefu wao, kufikiria hisia zao, na kuwasaidia wabaki wakiwa imara kiroho.

Makala ya Funzo ya 5 UKURASA 21-25

Kupitia nabii wake Sefania, Yehova alisema hivi: ‘Nitabadilisha lugha ya vikundi vya watu na kuwapa lugha safi.’ (Sef. 3:9) Jifunze maana ya “lugha safi.” Ona ni hatua gani unazoweza kufuata ili uijue vizuri na jinsi unavyoweza kutumia lugha hiyo ya pekee kumtukuza Yehova.

PIA KATIKA TOLEO HILI:

Neno la Yehova Liko Hai—Mambo Makuu Katika Barua kwa Wagalatia, Waefeso, Wafilipi, na Wakolosai

UKURASA WA 26

Je, Unakumbuka?

UKURASA WA 29

Wamishonari Ni Kama Nzige

UKURASA WA 30