Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Kwa Kweli Hilo Ni Jina la Mungu Ambalo Ni Takatifu na Kuu Zaidi”

“Kwa Kweli Hilo Ni Jina la Mungu Ambalo Ni Takatifu na Kuu Zaidi”

“Kwa Kweli Hilo Ni Jina la Mungu Ambalo Ni Takatifu na Kuu Zaidi”

Nicholas wa Cusa alisema maneno hayo katika mahubiri yake mwaka wa 1430. * Nicholas alipendezwa na habari mbalimbali. Kwa mfano, alijifunza Kigiriki, Kiebrania, falsafa, elimu ya dini, hesabu, na elimu ya nyota. Alikuwa mtaalamu wa sheria za Kanisa Katoliki akiwa na umri wa miaka 22. Katika mwaka wa 1448 aliteuliwa kuwa kadinali.

Miaka 550 hivi iliyopita, Nicholas wa Cusa alianzisha hospitali ya kuwatunzia wazee katika mji wa Kues, ambao sasa unaitwa Bernkastel-Kues, kilomita 130 hivi kusini mwa Bonn, huko Ujerumani. Kwa sasa maktaba ya Cusa iliyo na hati zaidi ya 310 iko katika jengo hilo. Moja ya hati hizo ni Kodeksi Cusanus 220 ambayo ina hotuba ya Cusa ya mwaka wa 1430. Katika hotuba hiyo, In principio erat verbum (Hapo Mwanzo Alikuwako Neno), Nicholas wa Cusa alitumia jina Yehova kama linavyoandikwa katika Kilatini, yaani, Iehoua. * Ukurasa wa 56 una maneno yafuatayo kuhusu jina la Mungu: “Ni jina ambalo Mungu amejipa. Ni Tetragramatoni, yaani, jina ambalo linafanyizwa kwa herufi nne. . . . Kwa kweli hilo ni jina la Mungu ambalo ni takatifu na kuu zaidi.” Maneno ya Nicholas wa Cusa yanaunga mkono kupatikana kwa jina la Mungu katika maandishi ya awali ya Maandiko ya Kiebrania.—Kut. 6:3.

Kodeksi hiyo ya karne ya 15 ni moja ya hati za zamani zaidi zilizopo ambamo Tetragramatoni inatafsiriwa kuwa “Iehoua.” Maandishi hayo ni uthibitisho mwingine wa kwamba tafsiri mbalimbali za jina la Mungu zinazofanana na “Yehova” ndizo zimejulikana zaidi kwa muda wa karne nyingi.

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 2 Nicholas wa Cusa aliitwa pia Nikolaus Cryfts (Krebs), Nicolaus Cusanus, na Nikolaus von Kues. Kues lilikuwa jina la mji wa Ujerumani mahali alipozaliwa.

^ fu. 3 Hotuba hiyo ilikuwa inatetea fundisho la Utatu.

[Picha katika ukurasa wa 16]

Maktaba ya Cusa