Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kumtumikia Mungu kwa “Moyo na Nafsi Moja”

Kumtumikia Mungu kwa “Moyo na Nafsi Moja”

Kumtumikia Mungu kwa “Moyo na Nafsi Moja”

WAYAHUDI na watu waliogeuzwa imani wanakutana pamoja na wanafunzi wa Yesu Kristo. Ni Sherehe ya Pentekoste, na wageni hao wamekuja Yerusalemu kutoka sehemu za mbali sana kama vile magharibi huko Roma na mashariki huko Parthia. Umati huo unazungumza lugha mbalimbali. Hata hivyo, wanafunzi wa Yesu ambao wanazungumza nao ni Wagalilaya. Baadhi ya wageni hao wanashtuka na kuuliza: “Imewezekanaje kwamba sisi, kila mmoja wetu, tunasikia lugha yake mwenyewe tuliyozaliwa nayo?”—Mdo. 2:8.

Mtume Petro anasimama na kueleza kusudi la muujiza ambao wanashuhudia. Umati huo unakubali papo hapo ujumbe huo. Maelfu ya wanafunzi wapya wanabatizwa! (Mdo. 2:41) Ingawa kutaniko linakua haraka, bado ni lenye umoja. Luka, mwandikaji wa Biblia anasema hivi: “Umati wa waliokuwa wameamini ulikuwa na moyo na nafsi moja.”—Mdo. 4:32.

Maelfu ya wale waliobatizwa siku ya Pentekoste mwaka wa 33 W.K. walitaka kubaki Yerusalemu kwa muda mrefu zaidi ili wajifunze kuhusu imani yao mpya. Hata hivyo, walipokuja hawakuwa na mpango wa kukaa Yerusalemu kwa muda mrefu. Hivyo, walifanya mpango wa muda wa kukusanya pesa. Waamini fulani walijitolea kuuza mali zao na kuleta mapato kwa mitume ili kuwagawia wale waliokuwa na uhitaji. (Mdo. 2:42-47) Walionyesha roho ya upendo na ukarimu kama nini!

Sikuzote Wakristo wa kweli wamekuwa na roho hiyo ya upendo na ukarimu. Leo, kutaniko la Kikristo linaendelea kumtumikia Yehova kwa umoja na kwa “moyo na nafsi moja.” Wakristo mmoja-mmoja wanatumia kwa ukarimu wakati, nguvu, na mali zao ili kuhubiri habari njema na kuendeleza faida za Ufalme wa Mungu.—Ona sanduku “Jinsi Ambavyo Wengine wanatoa Michango.”

[Sanduku katika ukurasa wa 6, 7]

JINSI AMBAVYO WENGINE WANATOA MICHANGO

MICHANGO KWA AJILI YA KAZI YA ULIMWENGUNI POTE

Wengi hutenga kiasi fulani cha pesa ambacho wao hutia katika masanduku ya michango yaliyoandikwa “Kazi ya Ulimwenguni Pote.”

Kila mwezi, makutaniko hutuma pesa hizo kwenye ofisi ya Mashahidi wa Yehova iliyo katika nchi yao. Pia, michango ya hiari ya pesa inaweza kutumwa moja kwa moja kwenye Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc., Attention Treasurer’s Office, 25 Columbia Heights, Brooklyn, New York 11201-2483, au kwenye ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova inayohudumia nchi yenu. Cheki za benki zinazotumwa kwenye anwani iliyoonyeshwa juu zinapaswa kuonyesha kwamba zitalipwa kwa shirika la “Watchtower.” Vito au vitu vingine vyenye thamani vinaweza kuchangwa vilevile. Barua fupi inayoonyesha kwamba vitu hivyo ni zawadi ya moja kwa moja inapaswa kuambatanishwa na michango hiyo.

MPANGO WA MICHANGO YENYE MASHARTI

Pesa zinaweza kutolewa kwa amana kwa shirika la Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania ili zitumiwe ulimwenguni pote. Hata hivyo, zinaweza kurudishwa iwapo zitaitishwa. Kwa habari zaidi, tafadhali wasiliana na Ofisi ya Mweka-Hazina kwa kutumia anwani iliyoonyeshwa hapa juu.

UTOAJI ULIOPANGWA

Mbali na zawadi za moja kwa moja za pesa, kuna njia nyinginezo za kutoa kwa ajili ya kazi ya Ufalme duniani pote. Njia hizo zinatia ndani:

Bima: Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania inaweza kutajwa kuwa mfaidikaji wa hati ya bima ya maisha au wa malipo ya kustaafu kazi au ya uzeeni.

Akiba za Benki: Akaunti za benki, hati za amana, au akiba za pesa za kustaafu za mtu mmoja-mmoja zinaweza kuwekwa zikiwa amana, au kulipwa wakati wa kifo kwa Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania, kulingana na matakwa ya benki za kwenu.

Hisa na Dhamana: Hisa na dhamana zinaweza kuchangwa kwa Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania zikiwa zawadi ya moja kwa moja.

Ardhi na Nyumba: Ardhi au nyumba zinazoweza kuuzwa zinaweza kutolewa zikiwa zawadi ya moja kwa moja au zawadi yenye masharti, yaani, mtoaji anaweza kuendelea kuishi humo hadi kifo chake. Julisha ofisi ya tawi katika nchi yako kabla ya kuchanga ardhi au nyumba.

Malipo-Mwaka: Huo ni mpango wa kutoa pesa, hisa, na amana, ziwe mali za shirika linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova. Yule anayetoa mchango huo, au mtu fulani aliyechaguliwa na mtoaji, hupata kiasi fulani cha pesa kila mwaka maishani mwake. Mtoaji hupunguziwa kodi ya serikali mwaka ule ambapo mpango huo unaanzishwa.

Wasia na Amana: Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania inaweza kuachiwa urithi wa mali au pesa kwa njia ya wasia halali, au Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania inaweza kutajwa kuwa mfaidikaji wa mkataba wa amana. Kuwa na amana inayofaidi tengenezo la kidini kunaweza kupunguza kwa kiasi fulani kodi ambayo hutozwa na serikali.

Kama vile usemi “utoaji uliopangwa” unavyodokeza, ili mtu atoe michango ya aina hii anapaswa kufanya mipango hususa. Broshua ya Kiingereza na Kihispania yenye kichwa Charitable Planning to Benefit Kingdom Service Worldwide imetayarishwa ili kuwasaidia watu wanaotamani kuendeleza kazi inayofanywa na Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote kwa njia ya utoaji uliopangwa. Broshua hiyo iliandikwa ili kutoa habari kuhusu njia mbalimbali za kutoa zawadi sasa au kama urithi mtu anapokufa. Baada ya kusoma broshua hiyo na kushauriana na washauri wao wa mambo ya sheria na kodi, watu wengi wameweza kusaidia kutegemeza kazi za kidini na za kutoa misaada za Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote, na kupunguziwa kodi wanapofanya hivyo. Unaweza kupata broshua hiyo kwa kuiomba moja kwa moja kutoka kwenye Charitable Planning Office.

Kwa habari zaidi, unaweza kuwasiliana na Charitable Planning Office, ama kwa kuandika ama kwa kupiga simu, kwenye anwani iliyoonyeshwa hapa chini, au unaweza kuwasiliana na ofisi ya Mashahidi wa Yehova ya nchi yenu.

Mashahidi wa Yehova

PO Box 21290

GPO Nairobi 00505

Kenya

Simu: (02) 3873211-20