Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Wamishonari Watiwa Moyo Wawe Kama Yeremia

Wamishonari Watiwa Moyo Wawe Kama Yeremia

Kuhitimu kwa Darasa la 125 la Gileadi

Wamishonari Watiwa Moyo Wawe Kama Yeremia

“DARASA hili la Gileadi ni la kihistoria,” akatangaza Geoffrey Jackson wa Baraza Linaloongoza. Alikuwa akihutubia watu 6,156 waliohudhuria programu ya kuhitimu ya darasa la 125 la Shule ya Gileadi (Watchtower Bible School of Gilead) mnamo Septemba 13, 2008 (13/9/2008). Kwa kuongezea wahitimu 56 wa darasa hili, Shule ya Gileadi imewatuma wamishonari zaidi ya 8,000 mpaka “sehemu ya mbali zaidi ya dunia”!—Mdo. 1:8.

Ndugu Jackson, mwenyekiti wa programu ya kuhitimu, aliuliza hivi: “Je, uaminifu utaboresha huduma yako?” Kisha akataja mambo manne ambayo yanajenga uaminifu: kuwa na mtazamo unaofaa, kuweka mfano mzuri, kutegemea kabisa Neno la Mungu unapofundisha, na kukazia fikira kulitangaza jina la Yehova.

David Schafer, ambaye anatumika katika Halmashauri ya Kufundisha, alizungumzia kichwa “Je, Utaelewa Kila Jambo?” Aliwahakikishia wanafunzi hao wa Gileadi kwamba wanaweza “kuelewa kila jambo” linalohitajiwa ili kutumika wakiwa wamishonari ikiwa wataendelea kumtafuta Yehova na kumtambua kwa unyenyekevu “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.”—Met. 28:5; Mt. 24:45.

Halafu, John E. Barr wa Baraza Linaloongoza alitoa hotuba yenye kichwa “Usiruhusu Chochote Kikutenganishe na Upendo wa Mungu.” Mashauri kama ya baba yaliyotolewa na Ndugu Barr yaliondoa wasiwasi wote ambao huenda wahitimu hao na wazazi wao walikuwa nao kuhusu mambo ambayo huenda wamishonari hao wapya wakakabili katika migawo yao. Ndugu Barr alieleza kwamba “hakuna mahali salama zaidi na penye starehe zaidi pa kukaa katika maisha yetu kuliko kukaa katika upendo wa Mungu.” Hakuna kitu kinachoweza kuwatenga wamishonari hao na upendo wa Mungu isipokuwa wajitenge wenyewe na Mungu.

Sam Roberson wa Idara ya Shule za Kitheokrasi aliwatia moyo wasikilizaji wavae “vazi bora zaidi kuliko mavazi yote.” Wahitimu hao wakijifunza mambo ambayo Yesu alifanya na kuyatumia katika maisha yao, wanaweza ‘kumvaa Bwana Yesu Kristo.’ (Rom. 13:14) Halafu, William Samuelson, mwangalizi wa Idara ya Shule za Kitheokrasi, akakazia jambo linalomfanya mtu aheshimike. Si maoni ya watu bali maoni ya Mungu ndiyo yanayomfanya mtu awe mwenye kuheshimika.

Michael Burnett, mmoja wa walimu, aliwahoji wanafunzi kuhusu mambo waliyojionea katika utumishi wa shambani. Ingawa wanafunzi wengi walitumwa katika maeneo yaliyohubiriwa sana walipokuwa katika Shule ya Gileadi huko Patterson, New York, walipata watu wanaopendezwa. Gerald Grizzle wa Ofisi ya Makusanyiko aliwahoji ndugu watatu wanaohudhuria Shule ya Washiriki wa Halmashauri ya Tawi. Maelezo yao yaliwasaidia wahitimu hao wa Gileadi kuelewa mambo ambayo watakabili katika migawo yao ya kigeni.

Hotuba yenye kichwa “Uwe Kama Yeremia” ilitolewa na David Splane wa Baraza Linaloongoza, mhitimu wa darasa la 42 la Gileadi. Ingawa Yeremia aliogopa mgawo wake, Yehova alimtia nguvu. (Yer. 1:7, 8) Mungu atawatia nguvu wamishonari hao wapya kama alivyomtia nguvu Yeremia. Ndugu Splane alisema hivi: “Ikiwa huelewani na mtu fulani, keti chini na uandike sifa kumi za mtu huyo ambazo unapenda. Na ikiwa huwezi kuandika sifa kumi, inamaanisha kwamba humjui vizuri sana mtu huyo.”

Yeremia alijidhabihu. Alipotaka kuacha mgawo wake, alisali, na Yehova akawa pamoja naye. (Yer. 20:11) Ndugu Splane alisema hivi: “Unapovunjika moyo, mwambie Yehova. Utashangaa kuona jinsi Yehova atakavyokusaidia.”

Mwishoni mwa programu hiyo ya kuhitimu, mwenyekiti aliwakumbusha wasikilizaji kwamba wahitimu wamejifunza njia mbalimbali za kujenga uaminifu. Wanapotoa ushahidi katika migawo yao, uaminifu wao utaboresha ushuhuda wao.—Isa. 43:8-12.

[Sanduku katika ukurasa wa 22]

TAKWIMU ZA DARASA

Idadi ya nchi ambazo zimewakilishwa: 6

Idadi ya nchi ambako wametumwa: 21

Idadi ya wanafunzi: 56

Wastani wa umri: 32.9

Wastani wa miaka katika kweli: 17.4

Wastani wa miaka katika huduma ya wakati wote: 13

[Picha katika ukurasa wa 23]

Darasa la 125 Lililohitimu la Shule ya Gileadi

Katika orodha iliyo chini, nambari za safu zinaanzia mbele kwenda nyuma, na majina yameorodheshwa kuanzia kushoto kwenda kulia katika kila safu.

(1) Hodgson, A.; Wall, A.; Beerens, K.; Hortelano, M.; Newman, L.; De Caso, A. (2) Jenkins, J.; Jarzemski, T.; Méndez, N.; Corona, V.; Canalita, L. (3) Fryer, H. ; Savage, M.; Tidwell, K.; Erickson, N.; Dyck, E.; McBeath, R. (4) Perez, L.; Puse, L.; Skidmore, A.; Young, B.; McBride, N.; Rondón, P.; Goodman, E. (5) Beerens, M.; Ferguson, J.; Pearson, N.; Chapman, L.; Wardle, J.; Canalita, M. (6) Perez, P.; De Caso, D.; Young, T.; Rondón, D.; Goodman, G.; Jenkins, M.; Dyck, G. (7) Corona, M.; Wall, R.; Puse, S; Méndez, F.; Jarzemski, S.; Savage, T. (8) Newman, C.; Ferguson, D.; Skidmore, D.; Erickson, T.; McBride, J.; Pearson, M.; Chapman, M. (9) Hodgson, K.; Wardle, A.; McBeath, A.; Tidwell, T.; Fryer, J.; Hortelano, J.