Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umefurahia kusoma matoleo ya hivi karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ona kama unaweza kujibu maswali yafuatayo:

• Kwa nini ni jambo la maana sana kudumisha utimilifu wetu wa Kikristo?

Kudumisha utimilifu wetu kunatuwezesha kuwa upande wa enzi kuu ya Yehova kwa sababu tunampenda na tunataka kuthibitisha kwamba Shetani ni mwongo. Mungu anatuhukumu kwa msingi wa utimilifu wetu, hivyo utimilifu wetu ni wa maana pia kwa tumaini letu la wakati ujao.—12/15, ukurasa wa 4-6.

• Taja vyeo fulani vinavyoonyesha daraka la Yesu katika kusudi la Mungu?

Mwana mzaliwa-pekee. Neno. Amina. Mpatanishi wa agano jipya. Kuhani Mkuu. Uzao ulioahidiwa.—12/15, ukurasa wa 15.

• Kwa nini Eliya alimwambia mtumishi wake atazame upande wa bahari nabii huyo alipokuwa akisali ili mvua inyeshe? (1 Fal. 18:43-45)

Eliya alionyesha kwamba alijua kuhusu mzunguko wa maji. Mawingu yaliyofanyizwa juu ya bahari yangepeperushwa juu ya nchi na kutokeza mvua.—1/1, ukurasa wa 15-16.

• Tunaweza kufanya nini ili tupate shangwe zaidi katika huduma yetu?

Tunaweza kuutayarisha moyo wetu, tukikazia fikira jinsi tunavyoweza kuwasaidia wengine. Tunaweza kuhubiri tukiwa na mradi wa kuanzisha mafunzo ya Biblia. Tukipata watu ambao hawapendezwi, tunaweza kuzungumzia mambo yanayowavutia watu katika eneo letu.—1/15, ukurasa wa 8-10.

• Je, ukoma unaotajwa katika Biblia ni sawa na ukoma uliopo leo?

Ukoma uliopo leo ambao unaambukizwa kupitia bakteria ulikuwapo katika nyakati za Biblia. (Law. 13:4, 5) Biblia inataja pia ukoma ambao ulionekana katika mavazi na nyumba. Huenda “ukoma” huo ulikuwa ukungu au kuvu ya aina fulani. (Law. 13:47-52)—2/1, ukurasa wa 19.

• Mafundisho ya Biblia yanapaswa kumfanya Mkristo awe na mtazamo gani kuelekea desturi za mazishi?

Ingawa Mkristo anaweza kuomboleza kwa sababu ya wapendwa wake waliokufa, anajua kwamba wafu hawajui lolote. Hata watu wasio waamini wakimshutumu, anaepuka desturi zinazohusiana na imani ya kwamba wafu wanaweza kuwa na uvutano kwa walio hai. Ili kuepuka matatizo, Wakristo fulani wanaandika maagizo kuhusu mipango yao ya mazishi.—2/15, ukurasa wa 29-31.

• Kulingana na Zaburi 1:1, tunapaswa kuepuka mambo gani matatu ili tuwe wenye furaha?

Mstari huo unataja “shauri la waovu,” “njia ya watenda-dhambi,” na “kiti cha wenye dhihaka.” Ndiyo, ili tuwe wenye furaha, tunahitaji kuwaepuka wale wanaodhihaki au kupuuza sheria za Mungu. Badala yake, tunapaswa kupendezwa na sheria ya Yehova.—3/1, ukurasa wa 17.

• Je, “kitabu cha Yashari” na “kitabu cha Vita vya Yehova” ni vitabu vya Biblia vilivyopotea? (Yos. 10:13; Hes. 21:14)

Hapana. Inaonekana kwamba ni hati ambazo hazikuongozwa na roho ya Mungu ambazo zilikuwapo katika nyakati za Biblia na zikarejelewa na waandikaji wa Biblia.—3/15, ukurasa wa 32.

• Ni badiliko gani kubwa lililofanywa katika tafsiri ya kisasa ya Biblia ya Kilatini?

Mwaka wa 1979, Papa John Paul wa Pili alitoa ruhusa ya kutumiwa kwa tafsiri mpya ya Kilatini inayoitwa Nova Vulgata. Tafsiri ya kwanza ilikuwa na jina la Mungu, Iahveh, katika maandiko fulani. (Kut. 3:15; 6:3) Hata hivyo, tafsiri ya pili iliyo rasmi ilipochapishwa mwaka wa 1986, neno Dominus [Bwana] lilitumiwa badala ya jina Iahveh.—4/1, ukurasa wa 22.