Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoa kwa Uchangamfu Kutoka Moyoni

Kutoa kwa Uchangamfu Kutoka Moyoni

Kutoa kwa Uchangamfu Kutoka Moyoni

KUHUSU kutoa, mtume Paulo aliandika hivi: “Kila mmoja na afanye kama alivyoazimia moyoni mwake,” na akaongezea hivi: “Si kwa kutopenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda mtoaji mchangamfu.” (2 Kor. 9:7) Yehova hamlazimishi yeyote kutegemeza ibada safi. Anawaruhusu watumishi wake waonyeshe kwamba wamejitoa kwake kupitia utoaji wao wa kutoka moyoni na mchangamfu. Katika historia yote, watu wake wametoa michango kwa uchangamfu. Hebu chunguza mifano mitatu.

Baada ya Yehova kuwaongoza Waisraeli kutoka Misri, aliwaagiza wajenge maskani. Vifaa vilihitajiwa, kwa hiyo, Waisraeli waliombwa watoe michango. Kwa kutii, “kila mtu ambaye moyo wake ulimsukuma” alileta dhahabu, fedha, vito, na vitu vingine. Watu walitoa kwa ukarimu sana hivi kwamba tangazo likatolewa ili waache kutoa.—Kut. 35:5, 21; 36:6, 7.

Karne nyingi baadaye, wakati hekalu lilipohitaji kujengwa, watu wa Mungu walikuwa na nafasi nyingine ya kuonyesha kwamba wanategemeza ibada safi. Mfalme Daudi mwenyewe alitoa mchango mkubwa ili kusaidia mradi huo na akawaalika wengine washiriki katika kutoa. Walifanya hivyo kwa kupenda. Kwa kweli, dhahabu na fedha iliyotolewa kama mchango ilikuwa na thamani ya dola zaidi ya bilioni 100 za Marekani ikikadiriwa kwa bei ya sasa! Watu walishangilia kwa sababu walimtolea Yehova michango kwa kupenda.—1 Nya. 29:3-9; 2 Nya. 5:1.

Wafuasi wa mapema wa Yesu Kristo vilevile walionyesha roho ya kutoa kwa shangwe. Katika siku ya Pentekoste mwaka wa 33 W.K., watu 3,000 hivi walibatizwa, na wengi wao hawakuwa wakaaji wa Yerusalemu. Ili kuwawezesha wale ambao walikuwa maskini wabaki katika jiji hilo ili wajifunze mengi kuhusu imani yao mpya, Wakristo walichanga mali zao kwa muda fulani. Ndugu waliuza vitu vyao wakawaletea mitume pesa ili wawasaidie wale ambao walikuwa na uhitaji. Kwa kweli, Yehova alifurahi sana kuona wakionyesha imani na upendo wao kwa njia hiyo!—Mdo. 2:41-47.

Leo, Wakristo wanaendelea kutegemeza ibada safi kwa kutoa wakati wao, nguvu zao, na michango yao ya kifedha kwa ukarimu na uchangamfu. Sanduku linalofuata linaonyesha njia fulani ambazo unaweza kutoa michango.

[Sanduku katika ukurasa wa 18, 19]

JINSI AMBAVYO WENGINE WANATOA MICHANGO

MICHANGO KWA AJILI YA KAZI YA ULIMWENGUNI POTE

Wengi wanatenga kiasi fulani cha pesa ambacho wanatia ndani ya masanduku ya michango yaliyoandikwa “Kazi ya Ulimwenguni Pote.”

Kila mwezi, makutaniko yanatuma pesa hizo kwenye ofisi ya Mashahidi wa Yehova inayosimamia kazi katika nchi yao. Pia, michango ya hiari ya pesa inaweza kutumwa moja kwa moja kwa Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc., Attention Treasurer’s Office, 25 Columbia Heights, Brooklyn, New York 11201-2483, au kwenye ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova inayosimamia kazi katika nchi yenu. (Michango ya hiari ambayo imeonyeshwa katika sehemu zilizo hapa chini inaweza pia kutumwa kwenye ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova inayosimamia kazi katika nchi yenu.) Cheki za benki zinazotumwa kwenye anwani iliyoonyeshwa hapo juu zinapaswa kuonyesha kwamba zitalipwa kwa “Watchtower.” Vito au vitu vingine vyenye thamani vinaweza kuchangwa vilevile. Barua fupi inayoonyesha kwamba vitu hivyo ni zawadi ya moja kwa moja inapaswa kuambatanishwa na michango hiyo.

MPANGO WA MICHANGO YENYE MASHARTI

Pesa zinaweza kutolewa kama amana kwa shirika la Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania ili zitumiwe ulimwenguni pote. Hata hivyo, zinaweza kurudishwa iwapo zitahitajiwa. Kwa habari zaidi, tafadhali wasiliana na Ofisi ya Mweka-Hazina kwa kutumia anwani iliyoonyeshwa hapo juu.

UTOAJI ULIOPANGWA

Mbali na zawadi za moja kwa moja za pesa, kuna njia nyingine za kutoa kwa ajili ya kazi ya Ufalme ya ulimwenguni pote. Njia hizo zinatia ndani:

Bima: Mtu anaweza kuandika kwamba Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania ndilo shirika ambalo litafaidika na hati ya bima ya maisha au mpango wa malipo ya uzeeni au ya kustaafu.

Akaunti za Benki: Akaunti za benki, hati za amana, au akiba za pesa za kustaafu za mtu mmoja-mmoja zinaweza kuwekwa zikiwa amana, au kulipwa wakati wa kifo kwa Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania, kulingana na matakwa ya benki za kwenu.

Hisa na Dhamana: Hisa na dhamana zinaweza kuchangwa kwa Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania zikiwa zawadi ya moja kwa moja au Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania linaweza kutajwa kuwa shirika ambalo litafaidika na hisa au dhamana hiyo kifo kikitokea.

Ardhi na Nyumba: Ardhi au nyumba zinazoweza kuuzwa zinaweza kutolewa zikiwa zawadi ya moja kwa moja au zawadi yenye masharti, yaani, mtoaji anaweza kuendelea kuishi humo hadi kifo chake. Wasiliana na ofisi ya tawi katika nchi yenu kabla ya kutoa ardhi au nyumba kama mchango.

Malipo ya Mwaka: Huo ni mpango wa kutoa pesa, hisa, na amana, ziwe mali ya shirika fulani linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova. Yule anayetoa mchango huo, au mtu fulani aliyechaguliwa na mtoaji, anapata kiasi fulani cha pesa kila mwaka katika maisha yake yote. Mtoaji anapunguziwa kodi ya serikali mwaka ambao mpango huo unaanzishwa.

Wasia na Amana: Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania inaweza kuachiwa urithi wa mali au pesa kwa njia ya wasia halali, au shirika la Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania linaweza kutajwa kuwa shirika ambalo litafaidika na mkataba wa amana. Serikali inaweza kupunguza kodi fulani kwa amana inayohusisha tengenezo la kidini.

Kama usemi “utoaji uliopangwa” unavyoonyesha, ili mtu atoe michango ya aina hiyo anapaswa kufanya mipango hususa. Broshua ya Kiingereza na Kihispania yenye kichwa Charitable Planning to Benefit Kingdom Service Worldwide imetayarishwa ili kuwasaidia watu wanaotamani kuendeleza kazi inayofanywa na Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote kwa njia ya utoaji uliopangwa. Broshua hiyo iliandikwa ili kutoa habari kuhusu njia mbalimbali za kutoa zawadi sasa au kama urithi mtu anapokufa. Baada ya kusoma broshua hiyo na kushauriana na washauri wao wa mambo ya kisheria au kodi, watu wengi wamesaidia kutegemeza utendaji wetu wa kidini na wa kutoa misaada ulimwenguni pote, na kupunguziwa kodi wanapofanya hivyo. Unaweza kupata broshua hiyo kwa kuomba nakala moja kwa moja kutoka kwa Charitable Planning Office.

Kwa habari zaidi, unaweza kuwasiliana na Charitable Planning Office. Unaweza pia kuandikia au kupiga simu kwa ofisi ya Mashahidi wa Yehova inayosimamia kazi katika nchi yenu.