Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Msichana Mdogo Mwenye Ukarimu

Msichana Mdogo Mwenye Ukarimu

Msichana Mdogo Mwenye Ukarimu

HIVI karibuni, bila kulazimishwa na mtu yeyote, msichana mwenye umri wa miaka tisa huko Brazili aligawanya mara mbili pesa ambazo alikuwa ameweka akiba—dola 18 na dola 25. Aliweka kiasi kilichokuwa kidogo katika sanduku la michango kwenye Jumba lao la Ufalme ili zitumiwe kulipia gharama za kutaniko. Kisha akatuma kiasi kilichokuwa kikubwa kwa ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova pamoja na barua fupi. Barua yake ilisema hivi: “Ninataka kutoa mchango huu kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote. Ninatamani kuwasaidia ndugu na dada wengi ulimwenguni pote wahubiri habari njema. Ninazitoa pesa hizi kwa sababu ninampenda sana Yehova.”

Wazazi wa msichana huyo mdogo wamemfundisha umuhimu wa kushiriki kibinafsi katika kazi ya kuhubiri kuhusu Ufalme. Wamemfundisha pia uhitaji wa ‘kumheshimu Yehova kwa vitu vyake vyenye thamani.’ (Met. 3:9) Kama msichana huyo mdogo, acheni sote tushiriki kwa bidii katika kuendeleza kazi ya Ufalme, katika eneo letu na ulimwenguni pote!