Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umefurahia kusoma matoleo ya hivi karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ona kama unaweza kujibu maswali yafuatayo:

• Ni nini kitakachokusaidia kuwafundisha watoto wako kutimiza madaraka yao?

‘Wawekee watoto wako kielelezo’ kuhusu jinsi ya kutimiza madaraka yao. (Yoh. 13:15) Uwe na usawaziko kuhusu mambo unayotaka watimize; mtoto anapoendelea kukua unaweza kutazamia atimize mengi zaidi katika mambo yanayohusu usafi, kutunza wakati, na kazi za shuleni. Toa maagizo hususa ili kumzoeza mtoto wako kutimiza madaraka yake.—5/1, ukurasa wa 19-20.

• kwa nini Mungu hakumwadhibu Haruni kwa sababu ya kutengeneza ndama wa dhahabu?

Haruni alivunja sheria ya Mungu kuhusu ibada ya sanamu. (Kut. 20:3-5) Hata hivyo, Musa alitoa dua kwa Mungu kwa ajili ya Haruni, na dua yake ilikuwa na “nguvu nyingi.” (Yak. 5:16) Haruni alikuwa na rekodi ya miaka mingi ya uaminifu. Na ingawa watu walimsihi Haruni atengeneze yule ndama, baadaye alionyesha kwamba moyo wake haukuwa pamoja nao kwa sababu alijiunga na wana wa Lawi katika kusimama upande wa Yehova. (Kut. 32:25-29)—5/15, ukurasa wa 21.

• Ofiri, ambako Biblia inataja kuwa chanzo cha dhahabu bora zaidi, ilikuwa wapi?

Ili kuleta dhahabu kutoka Ofiri, Sulemani alitengeneza meli huko Esion-geberi. (1 Fal. 9:26-28) Bandari hiyo ilikuwa upande wa juu wa Ghuba ya Aqaba karibu na eneo la Elat na Aqaba ya leo katika Bahari Nyekundu. Kwa hiyo, huenda Ofiri lilikuwa huko Arabia karibu na Bahari Nyekundu au kwenye pwani ya Afrika au pwani ya India.—6/1, ukurasa wa 15.

• “Zeri katika Gileadi” inamaanisha nini? (Yer. 8:22)

Mafuta ya zeri yalikuwa umajimaji wenye mafuta ambao ulikuwa na harufu nzuri uliotokana na mimea mbalimbali, ambayo ilipatikana katika maeneo mengi kutia ndani Gileadi, eneo lililokuwa upande wa mashariki wa Mto Yordani. Mafuta ya zeri yalikuwa na nguvu za kitiba, na hivyo yalipakwa kwenye vidonda. Hali ya kusikitisha ya taifa la Israeli ilipaswa kulichochea taifa hilo litafute tiba, lakini watu hawakufanya hivyo. (Yer. 8:9)—6/1, ukurasa wa 21-22.

• Ni nini kinachoweza kumsaidia Mkristo akabiliane na hali mwenzi wa ndoa anapofanya uzinzi?

Ikiwa mwenzi asiye na hatia amekuwa akijitahidi kuishi kulingana na kanuni za Biblia, hana sababu ya kuhisi kwamba ana hatia kwa sababu ya dhambi ya usaliti ya mwenzi wake mzinzi. Mungu anajua unahitaji kufarijiwa na kutiwa moyo. Huenda akaandaa faraja kupitia Wakristo wenzako.—6/15, ukurasa wa 30-31.

• Unaweza kufanya nini ili kumsaidia mtu aliye mgonjwa?

Msikilize kwa makini. (Mhu. 3:1, 7) Onyesha hisia-mwenzi na uwe mwenye kujali. (Rom. 12:15) Uwe mwenye kujenga na umsaidie. (Kol. 4:6; 1 Yoh. 3:18) Dumisha uhusiano wa karibu na rafiki yako. (Met. 17:17)—7/1, ukurasa wa 10-13.

• Tunajua jinsi gani kwamba Mungu hakuwa na mwanzo?

Musa alionyesha jambo hilo katika sala. (Zab. 90:2) Kwa kufaa, Yehova peke yake ndiye mwenye jina la cheo la kipekee, “Mfalme wa umilele.” (1 Tim. 1:17)—7/1, ukurasa wa 28.

• Unaweza jinsi gani kusitawisha ndani ya watoto wako tamaa ya kupenda kusoma?

Mazingira yenye upendo na mfano wa wazazi unaweza kusitawisha tamaa ya kupenda kusoma. Vilevile, wape vitabu vingi. Soma kwa sauti. Watie moyo washiriki, na mzungumzie mambo mnayosoma. Waombe watoto wako wasome kwa sauti huku ukisikiliza, na uwatie moyo waulize maswali.—7/15, ukurasa wa 26.

• Kwa nini Yesu hakwenda haraka kwa rafiki yake Lazaro aliyekuwa mgonjwa na kumponya?

Yesu alipofika, Lazaro alikuwa amekufa kwa siku nne. Kwa kungojea, Yesu alitoa ushahidi mzuri zaidi kumhusu Baba yake. Kwa hiyo, wengi wakawa waamini. (Yoh. 11:45)—8/1, ukurasa wa 14-15.

• “Mahali pa juu” palikuwa nini?

Katika visa vingi, panamaanisha maeneo yasiyo na paa yaliyokuwa juu ya vilima au mahali pengine palipofanyiwa ibada ya uwongo. Wakati mwingine, madhabahu, nguzo au miti mitakatifu, na vitu vingine vya ibada viliwekwa mahali mbalimbali ili kuendeleza mazoea ambayo yalikatazwa na Mungu. (Hes. 33:52)—8/1, ukurasa wa 23.