Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Tafakari Mambo Ambayo Yehova Amekufanyia

Tafakari Mambo Ambayo Yehova Amekufanyia

Tafakari Mambo Ambayo Yehova Amekufanyia

MUDA mfupi baada ya Yesu kufufuliwa, wawili kati ya wanafunzi wake walikuwa wakitembea kutoka Yerusalemu kwenda Emau. Masimulizi ya Injili ya Luka yanasema hivi: “Walipokuwa wakiongea na kujadiliana, Yesu akakaribia, akaanza kutembea pamoja nao; lakini macho yao yalizuiwa wasiweze kumtambua.” Kisha, Yesu akawaambia: “‘Ni mambo gani haya ambayo mnajadiliana kati yenu wenyewe mnapotembea?’ Nao wakasimama tuli wakiwa na nyuso zenye huzuni.” Kwa nini walihuzunika? Wanafunzi walikuwa na maoni ya kwamba Yesu angekomboa Israeli wakati huo kutoka chini ya utawala wa watu wasio Wayahudi, lakini hakuleta ukombozi huo. Badala yake, Yesu aliuawa. Basi, walihuzunika kwa sababu hiyo.—Luka 24:15-21; Mdo. 1:6.

Yesu alianza kuwasaidia wanafunzi kuelewa sababu. “Akaanzia Musa na Manabii wote, akawafasiria mambo yanayomhusu yeye mwenyewe katika Maandiko yote.” Kwa kweli, mambo mengi makubwa na yenye kutia imani nguvu yalikuwa yametukia wakati wa huduma ya Yesu! Wanafunzi hao walipokuwa wakisikiliza maelezo ya Yesu, mtazamo wao ulibadilika na wakawa na furaha badala ya huzuni. Baadaye jioni hiyo, walisema hivi: “Je, mioyo yetu haikuwa ikiwaka alipokuwa akisema nasi barabarani, alipokuwa akitufungulia Maandiko?” (Luka 24:27, 32) Tunajifunza somo gani kutokana na itikio la wanafunzi wa Yesu?

Tunahisi Jinsi Gani Mambo Tunayotarajia Yanapokosa Kutimia?

Wale wanafunzi wawili walipokuwa njiani kwenda Emau walihuzunika kwa sababu mambo ambayo walitarajia hayakuwa yametimia. Walikuwa na hisia ambayo inaelezwa katika andiko la Methali 13:12: “Tarajio lililocheleweshwa linafanya moyo uwe mgonjwa.” Vivyo hivyo, wengine wetu ambao wamekuwa wakimtumikia Yehova kwa uaminifu kwa miaka mingi walifikiri kwamba “dhiki kuu” ingekuwa imekuja na kupita kufikia sasa. (Mt. 24:21; Ufu. 7:14) Ni jambo linaloeleweka kwamba tarajio hilo ambalo halijatimia linaweza kusababisha huzuni kwa sasa.

Hata hivyo, kumbuka kwamba wale wanafunzi wawili walipata tena furaha yao baada ya Yesu kuwasaidia kukazia fikira unabii mbalimbali ambao tayari ulikuwa umetimizwa, hata wakati wa maisha yao. Tunaweza kuendelea kuwa na shangwe yetu ya moyoni na kupambana na hisia za kukata tamaa kwa kufanya hivyo. Mzee mmoja Mkristo mwenye uzoefu anayeitwa Michael alisema hivi: “Usikazie fikira mambo ambayo bado Yehova hajafanya. Badala yake, tafakari mambo ambayo tayari amefanya.” Hayo ni mashauri mazuri kama nini!

Mambo Ambayo Yehova Amefanya

Fikiria mambo fulani ya pekee ambayo tayari Yehova ametimiza. Yesu alisema hivi: “Yule anayeniamini, huyo pia atafanya kazi ambazo mimi hufanya; naye atafanya kazi kubwa kuliko hizi.” (Yoh. 14:12) Leo, kuliko wakati mwingine wowote, watumishi wa Mungu wanatimiza kazi kubwa zaidi za Kikristo. Watu zaidi ya milioni saba wanatazamia kuokoka ile dhiki kuu. Hebu wazia, hakujawahi kamwe kuwa na watumishi wengi sana hivyo waaminifu wa Yehova wanaohubiri kwa bidii katika nchi nyingi ulimwenguni pote! Yehova ametimiza maneno ya kinabii ya Yesu kuhusu “kazi kubwa kuliko hizi.”

Ni mambo gani mengine ambayo Yehova ametufanyia? Amewawezesha watu wanyoofu watoke katika ulimwengu mwovu, kwa njia ya mfano, na kuingia katika paradiso ya kiroho ambayo ameumba. (2 Kor. 12:1-4) Tenga wakati wa kutafakari mambo mbalimbali yaliyo katika paradiso hiyo ambayo tunaweza kufurahia. Kwa mfano, tazama maktaba yako ya nyumbani au ya Jumba la Ufalme. Chunguza Fahirisi ya Vichapo, au chunguza CD ya Watchtower Library. Sikiliza drama ya Biblia. Kumbuka mambo uliyosikia na kuona katika kusanyiko la karibuni. Kwa kuongezea, fikiria ushirika wenye kujenga ambao tunafurahia pamoja na ndugu na dada zetu Wakristo. Yehova amekuwa mkarimu kama nini katika kutuandalia chakula kingi cha kiroho na undugu wenye upendo—paradiso ya kiroho kwelikweli!

Mtunga-zaburi Daudi alisema hivi: “Wewe mwenyewe umefanya mambo mengi, Ee Yehova Mungu wangu, naam, kazi zako za ajabu na mawazo yako kutuelekea.” (Zab. 40:5) Ndiyo, tukitafakari mambo mazuri ajabu ambayo tayari Yehova ametufanyia na kutafakari mawazo yenye upendo aliyo nayo kutuelekea, tutapata nguvu zaidi za kuvumilia kwa uaminifu tunapomtumikia Baba yetu wa mbinguni, Yehova, kwa moyo wetu wote.—Mt. 24:13.

[Picha katika ukurasa wa 31]

Yesu aliwasaidia wanafunzi wake kutafakari mambo ambayo tayari Yehova alikuwa amewafanyia

[Picha katika ukurasa wa 32]

Kumbuka mambo uliyosikia na kuona katika kusanyiko la karibuni