Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umesoma kwa makini matoleo ya hivi karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ona kama unaweza kujibu maswali yafuatayo:

• Ni mambo gani matatu muhimu ambayo yanaweza kutusaidia kuendelea kuwa wanyoofu?

Mambo hayo ni: (1) Kusitawisha woga unaofaa kumwelekea Mungu. (1 Pet. 3:12) (2) Kusitawisha dhamiri iliyozoezwa na Biblia. (3) Kujitahidi kuendelea kuwa na hali ya kutosheka.—4/15, ukurasa wa 6-7.

• Tunajua jinsi gani kwamba kuchukua kwa uzito wote utumishi wetu kwa Yehova hakumaanishi kwamba tunapaswa kuonekana kuwa wakali sikuzote au kuepuka starehe?

Tunaweza kuchunguza mfano wa Yesu. Alifurahia chakula akiwa amestarehe pamoja na wengine. Tunajua kwamba hakuwa mkali kupita kiasi, na asiye mwenye urafiki. Watu wengine, kutia ndani watoto, walivutiwa naye na walistarehe walipokuwa pamoja naye.—4/15, ukurasa wa 10.

• Wenzi wa ndoa wanaweza kufanya nini ikiwa inaonekana kwamba uhusiano wao umedhoofika baada ya kupata watoto?

Kila mmoja anapaswa kumhakikishia mwenzake kwamba bado anampenda. Mume anapaswa kujitahidi kuondoa shaka lolote ambalo mke wake anaweza kuwa nalo. Na wote wawili wanapaswa kujitahidi kuwa na mawasiliano mazuri kuhusu hisia zao na mahitaji yao ya kimwili.—5/1, ukurasa wa 12-13.

• Mzeituni unaotajwa katika Waroma sura ya 11 ulifananisha nini?

Mzeituni huo unahusu sehemu ya pili ya mbegu ya Abrahamu, Israeli wa kiroho. Yehova ni kama mzizi na Yesu ni kama shina la mzeituni huo wa mfano. Wayahudi wengi wa asili walipomkataa Yesu, Watu wa Mataifa ambao waligeuka na kuwa waamini wangeweza kupandikizwa kwenye mti huo, hivyo kutokeza hesabu kamili ya sehemu ya pili ya mbegu ya Abrahamu.—5/15, ukurasa wa 22-25.

• Ni habari gani njema hasa ambayo tunaweza kuwapa maskini?

Habari hiyo njema ni hii: Mungu amemweka rasmi Yesu kuwa Mfalme. Yeye ndiye Mtawala anayestahili zaidi kumaliza umaskini. Kwa nini? Kwa sababu atatawala wanadamu wote na ana uwezo wa kutenda; anawahurumia maskini; na anaweza kumaliza chanzo cha umaskini, mwelekeo tuliozaliwa nao wa kuwa wachoyo.—6/1, ukurasa wa 7.

• Yesu alimaanisha nini alipomwambia Kayafa: “Wewe mwenyewe umesema”?—Mt. 26:63, 64.

Inaonekana kwamba usemi “wewe mwenyewe umesema” ulikuwa usemi wa kawaida kwa Wayahudi katika kukazia kwamba jambo lililosemwa lilikuwa la kweli. Kuhani Mkuu Kayafa alikuwa ameuliza kama Yesu alikuwa Kristo, Mwana wa Mungu. Jibu la Yesu lilikuwa: “Wewe mwenyewe umesema” jibu lililokazia kwamba jambo lililosemwa lilikuwa la kweli.—6/1, ukurasa wa 18.

• Je, wazao ambao mwanamume mkamilifu Yesu angeweza kuwa nao wangekuwa sehemu ya fidia au dhabihu ya ukombozi?

Hapana. Ingawa Yesu angeweza kutokeza mabilioni ya wazao wakamilifu, wazao hao hawangekuwa sehemu ya fidia. Uhai mkamilifu wa Yesu tu ndio uliolingana na uhai mkamilifu wa Adamu. (1 Tim. 2:6)—6/15, ukurasa wa 13.

• Wakristo wanaweza kuonyesha jinsi gani kwamba wanachukua kwa uzito onyo kuhusu walimu wa uwongo katika Matendo 20:29, 30?

Hawawakaribishi nyumbani mwao walimu wa uwongo au kuwasalimu. (Rom. 16:17; 2 Yoh. 9-11) Wakristo wanaepuka vitabu vya waasi-imani, vipindi vya televisheni vinavyohusisha waasi-imani, na Tovuti za Intaneti zenye mafundisho yao.—7/15, ukurasa wa 15-16.

• Ni nani anayepaswa kuwafundisha watoto kumhusu Mungu?

Kulingana na mashauri yaliyo katika Biblia, Baba na mama ndio wanaopaswa kufanya hivyo. (Met. 1:8; Efe. 6:4) Uchunguzi unaonyesha kwamba wazazi wote wawili wanapohusika, matokeo yanakuwa mazuri kwa watoto.—8/1, ukurasa wa 6-7.