Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unapata Shangwe Inayotokana na “Pendeleo la Kutoa kwa Fadhili”?

Je, Unapata Shangwe Inayotokana na “Pendeleo la Kutoa kwa Fadhili”?

Je, Unapata Shangwe Inayotokana na “Pendeleo la Kutoa kwa Fadhili”?

WAKRISTO wa karne ya kwanza huko Filipi walijulikana kwa sababu walitegemeza kwa ukarimu ibada ya kweli kupitia michango yao. Katika barua yake iliyoongozwa na roho ya Mungu, mtume Paulo aliwaandikia hivi: “Namshukuru Mungu wangu sikuzote kila mara ninapowakumbuka ninyi katika dua zangu zote kwa ajili yenu nyote, ninapoendelea kutoa dua yangu kwa shangwe, kwa sababu ya mchango ambao mmeutoa kwa ajili ya habari njema tangu siku ya kwanza mpaka sasa.” (Flp. 1:3-5) Paulo alikumbuka vizuri wakati Lidia na watu wa nyumba yake walipobatizwa na Lidia akaonyesha roho ya ukaribishaji-wageni kwa kusisitiza kwamba Paulo na wahubiri wenzake wakae nyumbani mwake.—Mdo. 16:14, 15.

Muda si muda, kutaniko jipya lililoanzishwa huko Filipi lilimtumia Paulo msaada mara mbili alipokaa kwa majuma kadhaa pamoja na waamini wenzake huko Thesalonike, umbali wa karibu kilomita 160. (Flp. 4:15, 16) Miaka michache baadaye, wakati ndugu wa Filipi na Makedonia walipokuwa wakikabili mateso na “umaskini mkubwa,” walisikia kuhusu uhitaji wa Wakristo waliokuwa wakiteswa huko Yerusalemu na wakataka kuwasaidia. Paulo alikiri kwamba kwa kweli walifanya “kupita uwezo wao halisi.” Hata hivyo, aliandika hivi: “Waliendelea kutuomba kwa kusihi sana wapate pendeleo la kutoa kwa fadhili.”—2 Kor. 8:1-4; Rom. 15:26.

Miaka kumi hivi baada ya Wafilipi kukubali Ukristo, bado walikuwa wakionyesha roho ileile ya ukarimu. Baada ya kusikia kuwa Paulo alikuwa amefungwa gerezani huko Roma, walimtuma Epafrodito umbali wa kilomita 1,287 kupitia baharini na maeneo mbalimbali akiwa na misaada kwa ajili ya mtume huyo. Kwa wazi, Wafilipi walitaka kumwandalia Paulo mahitaji ili aendelee kuwaimarisha akina ndugu na kuhubiri, hata alipokuwa gerezani.—Flp. 1:12-14; 2:25-30; 4:18.

Leo, Wakristo wa kweli huona kuwa ni pendeleo kutegemeza kazi ya kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi. (Mt. 28:19, 20) Wanaendeleza masilahi ya Ufalme kwa kutumia wakati wao, nguvu zao, na fedha zao. Sanduku lililo chini linaonyesha baadhi ya njia ambazo unaweza kushiriki katika kutegemeza kazi hii tuliyopewa na Mungu.

[Sanduku katika ukurasa wa 22, 23]

JINSI AMBAVYO WENGINE WANATOA MICHANGO

MICHANGO KWA AJILI YA KAZI YA ULIMWENGUNI POTE

Wengi wanatenga kiasi fulani cha pesa ambacho wanatia ndani ya masanduku ya michango yaliyoandikwa “Kazi ya Ulimwenguni Pote.”

Kila mwezi, makutaniko yanatuma pesa hizo kwenye ofisi ya Mashahidi wa Yehova inayosimamia kazi katika nchi yao. Pia, michango ya hiari ya pesa inaweza kutumwa moja kwa moja kwa Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc., Attention Treasurer’s Office, 25 Columbia Heights, Brooklyn, New York 11201-2483, au kwenye ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova inayosimamia kazi katika nchi yenu. (Michango ya hiari ambayo imeonyeshwa katika sehemu zilizo hapa chini inaweza pia kutumwa kwenye ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova inayosimamia kazi katika nchi yenu.) Vito au vitu vingine vyenye thamani vinaweza kuchangwa vilevile. Barua fupi inayoonyesha kwamba vitu hivyo ni zawadi ya moja kwa moja inapaswa kuambatanishwa na michango hiyo.

MPANGO WA MICHANGO YENYE MASHARTI

Pesa zinaweza kutolewa kama amana kwa shirika la Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania ili zitumiwe ulimwenguni pote. Hata hivyo, zinaweza kurudishwa iwapo zitahitajiwa. Kwa habari zaidi, tafadhali wasiliana na Ofisi ya Mweka-Hazina kwa kutumia anwani iliyoonyeshwa hapo juu.

UTOAJI ULIOPANGWA

Mbali na zawadi za moja kwa moja za pesa, kuna njia nyingine za kutoa kwa ajili ya kazi ya Ufalme ya ulimwenguni pote. Njia hizo zinatia ndani:

Bima: Mtu anaweza kuandika kwamba Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania ndilo shirika ambalo litafaidika na hati ya bima ya maisha au mpango wa malipo ya uzeeni au ya kustaafu.

Akaunti za Benki: Akaunti za benki, hati za amana, au akiba za pesa za kustaafu za mtu mmoja-mmoja zinaweza kuwekwa zikiwa amana, au kulipwa wakati wa kifo kwa Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania, kulingana na matakwa ya benki za kwenu.

Hisa na Dhamana: Hisa na dhamana zinaweza kuchangwa kwa Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania zikiwa zawadi ya moja kwa moja au Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania linaweza kutajwa kuwa shirika ambalo litafaidika na hisa au dhamana hiyo kifo kikitokea.

Ardhi na Nyumba: Ardhi au nyumba zinazoweza kuuzwa zinaweza kutolewa zikiwa zawadi ya moja kwa moja au zawadi yenye masharti, yaani, mtoaji anaweza kuendelea kuishi humo hadi kifo chake. Wasiliana na ofisi ya tawi katika nchi yenu kabla ya kutoa ardhi au nyumba kama mchango.

Malipo ya Mwaka: Huo ni mpango wa kutoa pesa, hisa, na amana, ziwe mali ya shirika fulani linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova. Yule anayetoa mchango huo, au mtu fulani aliyechaguliwa na mtoaji, anapata kiasi fulani cha pesa kila mwaka maisha yake yote. Mtoaji anapunguziwa kodi ya serikali mwaka ambao mpango huo unaanzishwa.

Wasia na Amana: Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania inaweza kuachiwa urithi wa mali au pesa kwa njia ya wasia halali, au shirika la Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania linaweza kutajwa kuwa shirika ambalo litafaidika na mkataba wa amana. Serikali inaweza kupunguza kodi fulani kwa amana inayohusisha tengenezo la kidini.

Kama usemi “utoaji uliopangwa” unavyoonyesha, ili mtu atoe michango ya aina hiyo anapaswa kufanya mipango hususa. Broshua ya Kiingereza na Kihispania yenye kichwa Charitable Planning to Benefit Kingdom Service Worldwide imetayarishwa ili kuwasaidia watu wanaotamani kuendeleza kazi inayofanywa na Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote kwa njia ya utoaji uliopangwa. Broshua hiyo iliandikwa ili kutoa habari kuhusu njia mbalimbali za kutoa zawadi sasa au kama urithi mtu anapokufa. Baada ya kusoma broshua hiyo na kushauriana na washauri wao wa mambo ya kisheria au kodi, watu wengi wamesaidia kutegemeza utendaji wetu wa kidini na wa kutoa misaada ulimwenguni pote, na kupunguziwa kodi wanapofanya hivyo. Unaweza kupata broshua hiyo kwa kuomba nakala moja kwa moja kutoka kwa Charitable Planning Office.

Kwa habari zaidi, unaweza kuwasiliana na Charitable Planning Office. Unaweza pia kutuma barua au kupiga simu kwa ofisi ya Mashahidi wa Yehova inayosimamia kazi katika nchi yenu.