Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umesoma kwa makini makala za hivi karibuni za Mnara wa Mlinzi? Ona ikiwa unaweza kujibu maswali yafuatayo:

Ni katika maana gani Sulemani anaweza kuwa kielelezo chenye kuonya kwetu?

Mungu alimbariki na kumtumia Mfalme Sulemani. Hata hivyo, wakati wa utawala wake, Sulemani alikiuka shauri la Mungu. Alimwoa binti mpagani wa Farao, akachukua wake wengi, na hatua kwa hatua akaruhusu wanawake wapagani wamwingize katika ibada ya uwongo. Tunahitaji kuepuka kukuza mielekeo au mitazamo mibaya hatua kwa hatua. (Kum. 7:1-4; 17:17; 1 Fal. 11:4-8)—12/15, ukurasa wa 10-12.

Kwa nini tunaweza kumwona Sara kuwa mwanamke mwenye kumwogopa Mungu na mke mwenye thamani?

Mungu alipomwagiza Abrahamu atoke Uru, ilimaanisha angeacha watu wa ukoo, marafiki, na maisha aliyozoea ili kuelekea mahali kusikojulikana. Hata hivyo, Sara aliunga mkono mpango huo, akiamini kwamba Mungu angembariki. Sara alimheshimu Abrahamu na kuonyesha sifa nzuri sana.—1/1, ukurasa wa 8.

Kwa nini Yehova alimwagiza Abrahamu amtoe mwana wake mpendwa kuwa dhabihu?

Ni muhimu kukumbuka kwamba kwa kweli Mungu hakumruhusu Abrahamu amtoe Isaka kuwa dhabihu. Hiyo ilikuwa njia ambayo Mungu aliitumia kuonyesha jinsi ambavyo, kwa gharama kubwa sana yeye mwenyewe, angemtoa Mwana wake, Yesu kuwa dhabihu.—1/1, ukurasa wa 23.

Ni nini kinachoonyesha kuwa tangu karne ya kwanza na kuendelea, kumekuwa na Wakristo wa kweli watiwa-mafuta nyakati zote duniani?

Katika mfano wa Yesu wa “ngano” na “magugu,” “mbegu nzuri” ilifananisha “wana wa ufalme.” (Mt. 13:24-30, 38) Magugu yangekua pamoja na ngano hadi wakati wa mavuno. Hivyo, ingawa hatuwezi kusema kwa hakika ni akina nani waliokuwa wa jamii ya ngano, ni lazima kumekuwa na watiwa-mafuta nyakati zote hadi wakati wetu.—1/15, ukurasa wa 7.

Ni matukio gani yatakayoongoza moja kwa moja kwenye Har–Magedoni?

Mataifa yatatoa tangazo muhimu la “Amani na usalama!” (1 The. 5:3) Serikali zitaishambulia dini ya uwongo. (Ufu. 17:15-18) Waabudu wa kweli watashambuliwa. Kisha mwisho utakuja.—2/1, ukurasa wa 9.

Tunawezaje kuushinda wivu?

Hatua zifuatazo zinaweza kutusaidia: Kujitahidi kukuza upendo na shauku ya kindugu, kushirikiana na watu wa Mungu, kujitahidi kufanya mema, ‘kushangilia pamoja na watu wanaoshangilia.’ (Rom. 12:15)—2/15, ukurasa wa 16-17.

Ni nani wanaozungumza lugha ya Kinahuatl, na ni nini kimefanywa kwa ajili yao?

Kinahuatl ilikuwa lugha ya kale ya Waazteki, na bado inazungumzwa na watu milioni 1.5 nchini Mexico. Mashahidi wanahubiri kwa kutumia lugha ya Kinahuatl, na baadhi ya machapisho yetu yanapatikana katika lugha hiyo.—3/1, ukurasa wa 13-14.

Ni kanuni gani tunazopaswa kukumbuka tunapotoa shauri?

Tambua hali halisi inayohusika. Epuka kujibu haraka. Kwa unyenyekevu, tumia Neno la Mungu. Ikiwezekana, tumia maktaba ya kitheokrasi. Epuka kuwafanyia wengine maamuzi.—3/15, ukurasa wa 7-9.

Yesu alimaanisha nini alipowaambia wasikilizaji wake waende kilometa mbili? (Mt. 5:41)

Wakati huo katika Israeli, Waroma waliokuwa wakiikalia nchi hiyo wangeweza kumlazimisha mtu afanye kazi fulani. Kwa kuwatia moyo wasikilizaji wake waende kilometa mbili, Yesu alimaanisha kwamba bila kinyongo, wasikilizaji wake walipaswa kufanya utumishi ambao wale waliokuwa kwenye mamlaka huenda kwa haki wangewadai.—4/1, ukurasa wa 9.