Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Nufaika kwa Kutumia Mbinu ya Kulinganisha na Kutofautisha

Nufaika kwa Kutumia Mbinu ya Kulinganisha na Kutofautisha

Je, hukubali kwamba Yesu ndiye Mwalimu mkuu zaidi aliyeishi duniani? Huenda umejaribu kufundisha ukitumia baadhi ya mbinu alizotumia, kama vile maswali na mifano. Hata hivyo, je, wajua kwamba mara nyingi alifundisha akitumia mbinu ya kulinganisha na kutofautisha mambo?

Watu wengi hufanya hivyo wanapoongea. Huenda ukafanya hivyo bila kufikiri. Unaweza kusema hivi: “Waliniambia kwamba matunda yote yameiva; lakini haya hayajaiva.” Au, “Alikuwa msichana mwenye haya sana, lakini sasa ana ujasiri.”

Katika hali kama hizo, unataja kwanza jambo la hakika; kisha jambo tofauti kabisa ukitumia maneno kama vile lakini, hata hivyo, badala ya, au kwa upande mwingine. Au huenda ukaonyesha tofauti kwa kulifafanua jambo au kwa kulikazia. Njia hiyo ya kuzungumza ni ya kawaida na inaweza kuwasaidia wengine kuelewa unachosema.

Hata ikiwa mbinu hiyo haitumiwi kwa ukawaida katika lugha au tamaduni fulani, ni vizuri tutambue umuhimu wa mbinu hiyo. Kwa nini? Kwa sababu inatumiwa sana katika Neno la Mungu lililoongozwa kwa roho. Mara nyingi Yesu alilinganisha na kutofautisha mambo. Kumbuka maneno haya aliyosema: “Watu huwasha taa na kuiweka, si chini ya kikapu cha kupimia, bali juu ya kinara cha taa.” “Sikuja kuharibu [Sheria], bali kutimiza.” “Ninyi mlisikia kwamba ilisemwa, ‘Usifanye uzinzi.’ Lakini mimi ninawaambia ninyi kwamba kila mtu ambaye anaendelea kumtazama mwanamke . . .” “Ilisemwa, ‘Jicho kwa jicho na jino kwa jino.’ Hata hivyo, mimi ninawaambia ninyi: Msimpinge yeye aliye mwovu; bali yeyote anayekupiga kofi kwenye shavu lako la kuume, mgeuzie lile lingine pia.”Mt. 5:15, 17, 27, 28, 38, 39.

Vitabu vingine vya Biblia hutumia mbinu hiyo pia. Mbinu hiyo inaweza kukusaidia kuelewa vizuri zaidi jambo au kukazia njia bora ya kufanya jambo fulani. Ikiwa wewe ni mzazi, fikiria jinsi mbinu hiyo inavyotumiwa katika andiko hili: “Akina baba, msiwe mkiwakasirisha watoto wenu, bali endeleeni kuwalea katika nidhamu na mwongozo wa akilini wa Yehova.” (Efe. 6:4) Kama mtume Paulo angeandika tu kwamba baba (au mama) anapaswa kumlea mtoto katika nidhamu ya Mungu, hilo lingekuwa jambo la hekima na la kweli. Hata hivyo, wazo hilo linaeleweka vizuri zaidi linapotofautishwa na wazo la ‘kutowakasirisha watoto, na badala yake kuwalea katika mwongozo wa akilini wa Yehova.’

Baadaye katika sura hiyo, Paulo aliandika hivi: “Tuna kushindana mweleka, si juu ya damu na mwili, bali juu ya . . . majeshi ya roho waovu katika mahali pa kimbingu.” (Efe. 6:12) Inaelekea kwamba ulinganifu huo  unakusaidia kuelewa kwamba una pigano kali sana. Si dhidi ya wanadamu tu bali dhidi ya majeshi ya roho waovu.

NUFAIKA KWA KUTUMIA MBINU YA KULINGANISHA NA KUTOFAUTISHA MAMBO

Katika kitabu hicho cha Waefeso, utapata maandiko mengine mengi ambamo Paulo alilinganisha na kutofautisha mambo. Kufikiria maandiko hayo kunaweza kutusaidia kuelewa alichomaanisha Paulo na kujua waziwazi jambo tunalopaswa kufanya.

Huenda ukafurahia na kunufaika ukichunguza chati inayoonyesha baadhi ya semi zinazolinganisha na kutofautisha mambo katika Waefeso 4 na 5. Unaposoma kila usemi, fikiria maisha yako. Jiulize hivi: ‘Kwa kweli nina mtazamo gani? Mimi hutendaje katika hali hiyo au inayofanana na hiyo? Ni mtazamo gani katika semi hizo ambao huenda wengine wakafikiri ninao?’ Ukitambua kwamba usemi fulani unaonyesha jambo unalohitaji kufanyia kazi, jitahidi kufanya hivyo. Nufaika kutokana na ulinganifu huo.

Au mnaweza kutumia chati hiyo katika ibada yenu ya familia. Kwanza, washiriki wote wa familia wanaweza kusoma semi hizo. Kisha mmoja wenu anaweza kutaja sehemu ya kwanza na kuwaacha wengine katika familia wajaribu kukumbuka jambo linalokaziwa katika sehemu ya pili. Kwa njia hiyo mnaweza kuwa na mazungumzo mazuri ya familia yanayoonyesha jinsi mnavyoweza kutumia kikamili sehemu ya pili ya kila usemi. Naam, kuchunguza semi hizo kwa njia hiyo kunaweza kuwasaidia wakubwa kwa wadogo kujiendesha kwa njia ya Kikristo katika familia na kwingineko.

Je, unakumbuka sehemu ya pili ya semi za kulinganisha?

Kadiri unavyojua umuhimu wa kulinganisha na kutofautisha mambo, ndivyo inavyokuwa rahisi zaidi kwako kutambua semi hizo katika Biblia, nazo zinaweza kukusaidia sana katika huduma yako ya Kikristo. Kwa mfano, unaweza kumwambia hivi mwenye nyumba: “Watu wengi husema kwamba kila mtu ana nafsi isiyoweza kufa, hata hivyo, ona jinsi Neno la Mungu linavyosema.” Au, unapoongoza funzo la Biblia, unaweza kuuliza hivi: “Watu wengi katika eneo hili wanaamini kwamba Mungu na Yesu ni mtu mmoja; lakini, tumeona Biblia inasema nini? Wewe unaamini nini?”

Naam, Maandiko yanatumia sana mbinu yenye kuelimisha ya kulinganisha na kutofautisha mambo inayoweza kutusaidia kutembea katika njia ya Mungu. Tunaweza kutumia mbinu hiyo kuwasaidia wengine kujua kweli ya Biblia.