Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umesoma kwa makini makala za hivi karibuni za Mnara wa Mlinzi? Angalia ikiwa unaweza kujibu maswali yafuatayo:

Yesu ‘aliwahubiria roho walio gerezani’ wakati gani? (1 Pet. 3:19)

Inaonekana kwamba muda fulani baada ya kufufuliwa, Yesu aliwatangazia roho hao waovu habari kuhusu hukumu waliyostahili kabisa ambayo watapata.—6/15, ukurasa wa 23.

Ni matatizo gani matatu utakayokabili unapojaribu kufanikisha ndoa ya pili?

Ni haya: kutolinganisha ndoa ya pili na ile ya kwanza; kushirikiana na marafiki wa zamani ambao hawamfahamu mwenzi wako wa pili; kumwamini mwenzi wako wa sasa hata ingawa mwenzi wako wa zamani hakuwa mwaminifu.—7/1, ukurasa wa 9-10.

Ni wakati gani Yesu anapohukumu watu kuwa kondoo au mbuzi? (Mt. 25:32)

Ni wakati Yesu atakapokuja kuwahukumu watu wakati wa dhiki kuu, baada ya kuharibiwa kwa dini ya uwongo.—7/15, ukurasa wa 6.

Waasi-sheria wanaotajwa katika mfano wa ngano na magugu watalia na kusaga meno yao wakati gani? (Mt. 13:36, 41, 42)

Watafanya hivyo wakati wa dhiki kuu watakapotambua kwamba hawawezi kuepuka uharibifu.—7/15, ukurasa wa 13.

Maneno ya Yesu kuhusu mtumwa mwaminifu na mwenye busara yangetimizwa wakati gani? (Mt. 24:45-47)

Yalianza kutimizwa baada ya mwaka wa 1914, wala si wakati wa Pentekoste ya 33 W.K. Katika mwaka wa 1919, mtumwa huyo aliwekwa rasmi juu ya watumishi wa nyumbani, wanaotia ndani Wakristo wote wanaolishwa kiroho.—7/15, ukurasa wa 21-23.

Yesu anamweka rasmi mtumwa mwaminifu juu ya mali zake zote wakati gani?

Atafanya hivyo wakati ujao, mtumwa huyo mwaminifu atakapopokea thawabu ya kimbingu wakati wa dhiki kuu.—7/15, ukurasa wa 25.

Je, Biblia haitaji majina ya watu fulani kwa sababu walikuwa wabaya au hawakuwa muhimu?

Hapana. Biblia haikutaja majina ya baadhi ya watu wazuri na wabaya pia. (Rut. 4:1-3; Mt. 26:18) Ni malaika wawili tu waaminifu wanaotajwa kwa majina katika Biblia.—8/1, ukurasa wa 10.

Mbali na nguvu kutoka kwa Mungu, ni nini kilichowasaidia Mashahidi 230 kuvumilia safari ndefu kutoka katika kambi ya mateso ya Sachsenhausen?

Ingawa walidhoofika kwa sababu ya njaa na magonjwa, waliendelea kutiana moyo ili waendelee na safari.—8/15, ukurasa wa 18.

Kwa nini simulizi la Waisraeli kuvuka Mto Yordani na kuingia Nchi ya Ahadi linatutia moyo?

Ingawa mto huo ulikuwa umefurika, Yehova alisimamisha maji ili watu wake wavuke. Bila shaka, hilo liliimarisha imani yao na kuwachochea kumtegemea Mungu, nasi tunatiwa moyo na simulizi hilo.—9/15, ukurasa wa 16.

Biblia inaonyesha nini kwa kutaja rangi mbalimbali?

Biblia inaonyesha kwamba Mungu anatambua jinsi hisia za wanadamu zinavyochochewa na rangi na kwamba rangi hutusaidia kukumbuka mambo.—10/1, ukurasa wa 14-15.

Unabii wa Mika 5:5 kuhusu watawala wadogo na wachungaji unatimizwa jinsi gani leo?

Tunaelewa kwamba wale “wachungaji saba na watawala wadogo wanane” wanaotajwa katika Mika 5:5 wanarejelea wazee waliowekwa rasmi kutanikoni, wanaowaimarisha watu wa Mungu ili kukabiliana na shambulizi litakalokuja lililotabiriwa.—11/15, ukurasa wa 20.

Kwa nini tunamhitaji Mungu?

Tunahitaji mwongozo unaofaa na majibu ya maswali muhimu maishani, na Mungu ndiye anayeweza kutupatia mambo hayo yote. Yuko tayari kutusaidia kuishi vizuri na kuwa na furaha, naye atatimiza ahadi zilizo katika Neno lake ili kutimiza jambo hilo.—12/1, ukurasa wa 4-6.