Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umesoma kwa makini makala za hivi karibuni za Mnara wa Mlinzi? Ona ikiwa unaweza kujibu maswali yafuatayo:

Mwana-kondoo wa Pasaka alichinjwa wakati gani katika Nisani 14?

Tafsiri fulani za Biblia husema kwamba mwana-kondoo angechinjwa “katikati ya zile jioni mbili,” kumaanisha wakati wa jioni au giza linapoanza kuingia, yaani, baada ya jua kutua lakini kabla ya giza kuingia. (Kut. 12:6)12/15, ukurasa wa 18-19.

Vijana wanaweza kutumia kanuni gani za Biblia kufanya maamuzi ya hekima?

Kanuni hizo tatu ni (1) Tafuta kwanza Ufalme wa Mungu na uadilifu wake. (Mt. 6:19-34) (2) Pata furaha kwa kuwatumikia wengine. (Mdo. 20:35) (3) Furahia kumtumikia Yehova ukiwa kijana. (Mhu. 12:1)1/15, ukurasa wa 19-20.

Ni wapanda-farasi gani wanne walio mwendoni tangu mwaka wa 1914?

Yesu, mpandaji wa farasi mweupe, alimwondoa Shetani na mashetani wake kutoka mbinguni. Mpandaji wa farasi wa rangi ya moto anafananisha vita vinavyowatesa wanadamu. Mpandaji wa farasi mweusi anafananisha njaa. Mpandaji wa farasi wa kijivu analeta kifo kwa pigo na kumaliza mamilioni. (Ufu. 6:2-8)2/1, ukurasa wa 6-7.

“Ndoa ya Mwana-Kondoo” itafanywa wakati gani? (Ufu. 19:7)

“Ndoa ya Mwana-Kondoo” itafanywa baada ya Mfalme, Yesu Kristo, kumaliza ushindi wake, yaani, baada ya Babiloni Mkubwa kuharibiwa na vita vya Har–Magedoni kupiganwa.—2/15, ukurasa wa 10.

Kwa nini Wayahudi katika siku za Yesu walikuwa ‘wakimtarajia’ Masihi? (Luka 3:15)

Hatujui kwa uhakika ikiwa Wayahudi wa karne ya kwanza walielewa unabii wa Danieli kuhusu Masihi kama tunavyouelewa. (Dan. 9:24-27) Hata hivyo, huenda walisikia tangazo la malaika kwa baadhi ya wachungaji au kile alichosema nabii wa kike aliyeitwa Ana baada ya kumwona Yesu alipoletwa hekaluni akiwa mtoto mchanga. Pia, wanajimu walikuja kumtafuta “yule mfalme wa Wayahudi aliyezaliwa.” (Mt. 2:1, 2) Baadaye, Yohana Mbatizaji alionyesha kwamba Kristo angetokea baada ya muda mfupi.2/15, ukurasa wa 26-27.

Tutafanya nini ili Ndiyo yetu isiwe Siyo? (2 Kor. 1:18)

Kwa kweli, huenda tukashindwa nyakati fulani kutimiza ahadi yetu kwa sababu ya hali zisizoepukika. Hata hivyo, tukiweka mkataba au kutoa ahadi, tunapaswa kufanya yote tuwezayo ili kutimiza ahadi hiyo.3/15, ukurasa wa 32.

Tunawezaje kupinga kishawishi cha kutazama ponografia?

Hatua hizi tatu zitatusaidia (1) Tukiona picha inayoamsha hamu ya ngono, tunapaswa kutazama kando mara moja. (2) Tulinde mawazo yetu kwa kufikiria mambo yanayofaa na kusali kwa Mungu. (3) Tulinde hatua zetu kwa kuepuka sinema au kutazama ponografia kwenye Intaneti.4/1, ukurasa wa 10-12.

Matokeo yatakuwa nini Mkristo akiiacha familia yake na kuhamia nchi nyingine ili kutafuta pesa?

Wazazi wanapoamua kuishi mbali na watoto wao, watoto wanaweza kuathiriwa kihisia na kimaadili. Huenda watoto wasitake kuwaona wazazi wao wanapowatembelea. Watu wanaoishi mbali na wenzi wao wa ndoa huenda wakashawishiwa kufanya uzinzi.4/15, ukurasa wa 19-20.

Kwa nini wahalifu walivunjwa miguu kabla ya kuuawa juu ya mti wa mateso?

Waroma waliua baadhi ya wahalifu juu ya mti wa mateso. Wayahudi waliomba kwamba miguu ya wahalifu waliotundikwa karibu na Yesu ivunjwe. Kufanya hivyo kungefanya washindwe kupumua, na hivyo kufa haraka. Hivyo, hawangehitaji kubaki juu ya mti wa mateso usiku mzima. (Kum. 21:22, 23)5/1, ukurasa wa 11.

Tunahitaji kukumbuka maswali gani manne tunapohubiria watu katika huduma yetu?

Ninahubiria nani? Ninawahubiria wakiwa wapi? Ninawahubiria wakati gani? Nitatumia utangulizi gani?5/15, ukurasa wa 12-15.

Kuvuta sigara kunasababisha madhara gani?

Katika karne iliyopita, uvutaji wa sigara uliua watu 100,000,000. Kila mwaka, uvutaji wa sigara huua watu 6,000,000.6/1, ukurasa wa 3.