MNARA WA MLINZI—TOLEO LA FUNZO Agosti 2014

Toleo hili lina makala za funzo kwa ajili ya Septemba 29 hadi Oktoba 26, 2014.

Je, Unapata ‘Chakula kwa Wakati Unaofaa’?

Je, ni lazima mtu apate habari zote ambazo mtumwa mwaminifu anaandaa ili aendelea kuwa imara kiroho?

Wanawake Wanatimiza Sehemu Gani Katika Kusudi la Yehova?

Kumwasi Mungu kumewaathirije wanaume na wanawake? Chunguza mifano ya baadhi ya wanawake waaminifu wa nyakati za kale. Pia, jifunze jinsi wanawake Wakristo wanavyoshiriki katika kazi ya Mungu leo.

Tumia Neno la Mungu​—Liko Hai!

Mashahidi wote wa Yehova wanataka kuwa stadi katika huduma. Chunguza baadhi ya mapendekezo ya kutumia Neno la Mungu lenye nguvu pamoja na trakti zetu tunapohubiri.

Jinsi Yehova Anavyotukaribia

Tunahitaji kuwa na uhusiano wa karibu na Yehova. Jifunze jinsi fidia na Biblia inavyothibitisha kwamba Yehova anatuvuta kwake.

Sikia Sauti ya Yehova Popote Ulipo

Jifunze umuhimu wa kusikiliza sauti ya Yehova na kuwasiliana naye. Makala hii itatusaidia kuona jinsi tunavyoweza kuepuka kukengeushwa na Shetani na mielekeo yetu ya dhambi na hivyo kutomsikiliza Yehova.

‘Rudi na Uwatie Nguvu Ndugu Zako’

Ikiwa ndugu aliyetumika awali akiwa mzee lakini sasa hana pendeleo hilo, anawezaje ‘kujitahidi tena kufikia cheo cha mwangalizi’?

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Je, Yesu alikuwa akizungumzia ufufuo wa wale watakaoishi duniani aliposema wale watakaofufuliwa “hawaoi wala hawaolewi?”

HIFADHI YETU YA VITU VYA KALE

“Eureka Drama” Iliwasaidia Wengi Kupata Kweli ya Biblia

Toleo hilo lililofupishwa la “Photo-Drama of Creation” lingeweza kuonyeshwa katika maeneo ya mashambani, bila kutumia umeme.