MNARA WA MLINZI—TOLEO LA FUNZO Septemba 2014

Toleo hili lina makala za funzo za mwezi wa Oktoba 27 hadi Novemba 30, 2014.

Je, ‘Unajitahidi Kufikia’ Mapendeleo?

Unawezaje kufanya hivyo kwa njia inayofaa?

Je, Unasadiki Kwamba Una Kweli? Kwa Nini?

Makala hii itazungumzia baadhi ya sababu zinazofanya watu wengi wakubali kwamba Mashahidi wa Yehova wana kweli. Tutachunguza pia sababu kwa nini Mashahidi wanasadiki kwamba wana kweli.

Mtumikie Mungu kwa Ushikamanifu Licha ya “Dhiki Nyingi”

Kila mtu hupatwa na dhiki kwa sababu ya kuishi katika ulimwengu wa Shetani. Shetani hutumia mbinu gani kutushambulia? Tunawezaje kujitayarisha kukabiliana nazo?

Wazazi—Wachungeni Watoto Wenu

Wazazi wana jukumu la kuwalea watoto wao “katika nidhamu na mwongozo wa akilini wa Yehova.” (Waefeso 6:4) Makala hii inazungumzia njia tatu ambazo wazazi wanaweza kutumia kuwachunga watoto wao na kuwasaidia kumpenda Yehova.

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Je, andiko la Zaburi 37:25 na Mathayo 6:33 yanamaanisha kwamba Yehova hataruhusu kamwe Mkristo kukosa chakula?

Adui wa Mwisho, Kifo, Aangamizwa

Wanadamu huteseka sana kwa sababu ya kifo na hali zinazokisababisha. Kwa nini watu wanakufa? ‘Adui wa mwisho, kifo,’ ataangamizwaje? (1 wakorintho 15:26) Tazama jinsi majibu ya maswali hayo yanavyoonyesha haki, hekima, na hasa upendo wake.

Wakumbuke Watumishi wa Wakati Wote

Waabudu wengi wa Yehova hujitahidi sana katika utumishi wa wakati wote. Tunawezaje kukumbuka ‘kazi yao ya uaminifu’ na ‘kazi yao ya jasho yenye upendo’?—1 Wathesalonike 1:3.