Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

‘Endeleeni Kuwaheshimu Sana Watu wa Namna Hiyo’

‘Endeleeni Kuwaheshimu Sana Watu wa Namna Hiyo’

TANGU mwaka wa 1992, Baraza Linaloongoza limewaweka rasmi wazee wakomavu na wenye uzoefu ili wasaidie kazi katika halmashauri zake mbalimbali. * Wasaidizi hao, ambao ni miongoni mwa “kondoo wengine,” wanalisaidia sana Baraza Linaloongoza. (Yoh. 10:16) Wanahudhuria mikutano ya kila juma ya halmashauri wanazotumikia, nao hutoa maelezo na mapendekezo yao. Baraza Linaloongoza ndilo hufanya uamuzi wa mwisho, lakini wasaidizi wao hutekeleza maamuzi hayo na kutimiza mgawo wowote wanaopewa. Pia, wao huandamana na washiriki wa Baraza Linaloongoza kwenye makusanyiko ya eneo ya pekee na ya kimataifa. Isitoshe, wanaweza kupewa mgawo wa kutembelea ofisi za tawi wakiwa wawakilishi wa makao makuu.

Msaidizi mmoja ambaye ametumikia tangu mpango huu ulipoanzishwa, anasema hivi: “Ninapotimiza migawo yangu, ninalisaidia Baraza Linaloongoza kutimiza kikamili majukumu yake.” Ndugu mwingine aliyetumikia kwa miaka 20 akiwa msaidizi, anasema hivi: “Imekuwa heshima kubwa sana kwangu na sikuwahi kutarajia jambo hilo.”

Baraza Linaloongoza limewakabidhi wasaidizi wake majukumu mengi na linathamini kazi bora inayofanywa na ndugu hao washikamanifu na wenye bidii. Acheni sote ‘tuendelee kuwaheshimu sana watu wa namna hiyo.’—Flp. 2:29.

^ fu. 2 Tazama sanduku lenye kichwa “Jinsi Baraza Linaloongoza Linavyoshughulikia Mambo ya Ufalme” katika sura ya 12 ya kitabu Ufalme wa Mungu Unatawala! ili kupata muhtasari wa majukumu ya halmashauri sita za Baraza Linaloongoza.