Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Machi 22, 2008—Siku ya Kukumbuka

Machi 22, 2008—Siku ya Kukumbuka

Machi 22, 2008—Siku ya Kukumbuka

Jioni iliyotangulia kifo chake, Yesu aliwapa mitume wake mkate usiotiwa chachu na kikombe cha divai na kuwaagiza wale na kunywa. Pia aliwaambia: “Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.”—Luka 22:19.

Mwaka huu, ukumbusho wa tukio hilo utakuwa Jumamosi, Machi 22, baada ya jua kushuka. Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote watakutana usiku huo wa pekee ili kuadhimisha Ukumbusho huo kama Yesu alivyoamuru. Tunakukaribisha kwa uchangamfu ujiunge nasi kushuhudia tukio hilo. Tafadhali wasiliana na Mashahidi wa Yehova katika eneo lenu ili ujue wakati na mahali pa mkutano huo.