Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Wajua?

Je, Wajua?

Je, Wajua?

Kwa nini Pontio Pilato aliingiwa na woga aliposikia shtaka la kwamba Yesu “alijifanya mwenyewe kuwa mwana wa Mungu”?—Yohana 19:7.

Baada ya kifo cha Kaisari Yulio, Baraza la Roma lilimtangaza mtawala huyo kuwa mungu. Baadaye, Octavian, mwana wake wa kambo ambaye pia alikuwa mrithi wake, alitangazwa kuwa divi filius, yaani, “Mwana wa Mungu.” Maneno hayo ya Kilatini yakawa jina takatifu la cheo la maliki. Hilo linaweza kuthibitishwa na maandishi mengi yaliyo katika madhabahu, nguzo, na sarafu za Roma. Wayahudi walipomshtaki Yesu kwa kujifanya mwenyewe kuwa “mwana wa Mungu,” kwa kweli, walikuwa wakimshtaki kwamba amejitwalia cheo cha kiserikali, kosa sawa na la uhaini.

Kufikia wakati Yesu aliposhtakiwa, Tiberio alikuwa amerithi cheo cha divi filius. Maliki huyo aliogopwa sana kwa sababu ilijulikana kwamba angemuua yeyote aliyemwona kuwa adui yake. Hivyo, Wayahudi walipodokeza kwamba Pilato angekosa ushikamanifu kwa Kaisari ikiwa hangemhukumu Yesu, Gavana huyo Mroma ‘aliogopa zaidi.’ Hatimaye, baada ya kushinikizwa sana alisalimu amri na kuagiza Yesu auawe.—Yohana 19:8, 12-16.

Kwa nini Zekaria alitabiri kuanguka kwa Tiro muda mrefu baada ya jiji hilo kuharibiwa na Wababiloni?

Kwa kweli, Tiro la kale lililokuwa katika pwani ya Mediterania, lilifanyizwa kwa sehemu mbili. Sehemu moja ilikuwa barani na ile nyingine ilikuwa kisiwani.

Wakati fulani, wakaaji wa Tiro waliwatendea Waisraeli vizuri. Lakini baadaye, Tiro likawa na ufanisi na kumwasi Yehova Mungu, hata wakaiba dhahabu na fedha katika hekalu lake na kuwauza baadhi ya watu wake utumwani. (Yoeli 3:4-6) Kwa sababu hiyo, walihukumiwa vikali na Yehova. Kupitia nabii wake, Yehova alitabiri kwamba Tiro lingeanguka mikononi mwa Nebukadreza Mfalme wa Babiloni, ambaye alileta majeshi yake Tiro baada ya kuharibu Yerusalemu mwaka wa 607 K.W.K.—Isaya 23:13, 14; Yeremia 27:2-7; Ezekieli 28:1-19.

Wakitazamia kushindwa, watu wa Tiro walichukua mali zao na kukimbilia jiji la kisiwani. Wababiloni waliharibu jiji la barani. Karibu miaka 100 baadaye, Yehova alimwongoza kwa roho nabii wake Zekaria atangaze hukumu Yake juu ya Tiro: “Tazama! Yehova mwenyewe atamfukuza, naye hakika atalipiga na kuliangusha baharini jeshi lake; naye mwenyewe atateketezwa motoni.”—Zekaria 9:3, 4.

Mnamo 332 K.W.K., jiji la kisiwani liliharibiwa na Aleksanda Mkuu, na hivyo kutimiza unabii wa Zekaria. Ili kuliharibu jiji hilo, Aleksanda alijenga barabara yenye urefu wa mita 800 juu ya maji kutoka barani hadi kisiwani akitumia mbao na mawe ya magofu ya jiji la barani la Tiro. Hilo pia lilikuwa limetabiriwa na Ezekieli.—Ezekieli 26:4, 12.

[Picha katika ukurasa wa 27]

“Kuzingirwa kwa Tiro”

[Hisani]

Drawing by Andre Castaigne (1898-1899)