Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Yesu Awashangaza Wasikilizaji Wake

Yesu Awashangaza Wasikilizaji Wake

Kwa Ajili ya Vijana Wetu

Yesu Awashangaza Wasikilizaji Wake

Maagizo: Fanya zoezi hili katika mazingira matulivu. Unaposoma maandiko, jiwazie ukiwa katika matukio yanayozungumziwa. Wazia kikao. Sikia sauti. Hisi kama wahusika wakuu wanavyohisi. Wazia kwamba masimulizi haya ni halisi kabisa.

CHUNGUZA TUKIO HILI.—SOMA LUKA 2:41-47.

Unafikiria ni mambo ya aina gani yaliyokuwa yakizungumziwa kama inavyofafanuliwa kwenye mstari wa 46?

․․․․․

CHIMBA ZAIDI.

Unafikiria ni kwa nini Yesu angeweza kuzungumza na viongozi wa kidini akiwa na umri mchanga hivyo? Je, ni kwa sababu tu alikuwa mkamilifu, au kulikuwa na sababu nyingine?

․․․․․

CHUNGUZA TUKIO HILI.—SOMA LUKA 2:48-52.

Unafikiri Yesu alikuwa na mtazamo gani alipouliza: “Kwa nini mlilazimika kunitafuta?”

․․․․․

wa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba Yesu hakuzungumza na wazazi wake kwa kejeli au kwa kukosa heshima?

․․․․․

CHIMBA ZAIDI.

Kwa nini haishangazi kwamba Yosefu na Maria walihangaika?

․․․․․

Ingawa Yesu alikuwa mkamilifu, kwa nini alihitaji kuendelea kujitiisha kwa wazazi wake?

․․․․․

Je, unafikiri kwamba inawezekana Yesu aliaibika kusahihishwa mbele ya watu waliovutiwa naye?

․․․․․

TUMIA MAMBO ULIYOJIFUNZA. ANDIKA MAMBO ULIYOJIFUNZA KUHUSU . . .

Kujitiisha.

․․․․․

Umuhimu wa kujipatia ujuzi wa Biblia ukiwa kijana.

․․․․․

NI MAMBO GANI KATIKA SIMULIZI HILI LA BIBLIA AMBAYO YAMEKUGUSA MOYO SANA, NA KWA NINI?

․․․․․