Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Wakati wa Kufanya Uamuzi

Wakati wa Kufanya Uamuzi

Wakati wa Kufanya Uamuzi

“Mungu akamuumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimuumba; mwanamume na mwanamke aliwaumba.”—Mwanzo 1:27.

MANENO hayo yanayojulikana sana yaliyo katika kurasa za kwanza za Biblia yanaonyesha moja kati ya mambo makuu zaidi ambayo Mungu ‘amefanya yawe yenye kupendeza kwa wakati wake,’ yaani, kuwaumba wenzi wawili wakamilifu, Adamu na Hawa. (Mhubiri 3:11) Akiwa Muumba wao, Yehova Mungu aliwaambia hivi: “Zaeni, muwe wengi, mjaze dunia na kuitiisha, na mtawale samaki wa baharini na viumbe vinavyoruka vya mbinguni na kila kiumbe hai kinachotambaa juu ya dunia.”—Mwanzo 1:28.

Kwa maneno hayo, Mungu aliwajulisha wenzi wawili wa kwanza kusudi lake. Walipaswa kuzaana na kuitunza dunia, wakiifanya iwe paradiso kwa ajili yao na wazao wao. Hawakuwa wamepangiwa siku ambayo watakufa. Badala yake, Mungu aliwaahidi kitu kizuri sana. Kwa kufanya uamuzi unaofaa na kuendelea kumtii Mungu, wangeweza kuishi milele kwa furaha na amani ya kweli.

Walifanya uamuzi usiofaa na kwa sababu hiyo wanadamu wote wanazeeka na kufa. Mzee wa ukoo Ayubu alisema hivi: “Mwanadamu, aliyezaliwa na mwanamke, ana maisha mafupi na yenye kujaa msukosuko.” (Ayubu 14:1) Mambo yaliharibikia wapi?

Biblia inaeleza hivi: “Kupitia mtu mmoja dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia dhambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya dhambi.” (Waroma 5:12) ‘Mtu huyo mmoja’ ni Adamu ambaye alikataa kutii kimakusudi amri ya Mungu iliyokuwa wazi na rahisi. (Mwanzo 2:17) Kwa kupenda kwake, Adamu alipoteza nafasi ya kuishi milele katika dunia iliyo paradiso. Pia, aliwapotezea wazao wake urithi wenye thamani na kuwapitishia laana ya dhambi na kifo. Ni kana kwamba kila kitu kilikuwa kimepotea. Je, kulikuwa na matumaini yoyote?

Wakati wa Kufanya Mambo Upya

Maelfu ya miaka baadaye, mtunga-zaburi aliongozwa na roho kuandika hivi: “Waadilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake.” (Zaburi 37:29) Kama uhakikisho kwamba ahadi aliyotoa katika bustani ya Edeni itatimia, Neno la Mungu linaeleza yale ambayo Mungu atafanya hivi karibuni: “Atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.” Kisha Mungu mwenyewe anasema: “Tazama! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.”—Ufunuo 21:4, 5.

Kwa kuwa kuna wakati uliowekwa kwa ajili ya kila kitu, swali ambalo linazuka ni, Wakati huo wa kufanya mambo upya ili ahadi nzuri ambazo Mungu ametoa zitimie utakuja lini? Mashahidi wa Yehova, ambao ndio wachapishaji wa gazeti hili, wamekuwa wakijitahidi sana kuwajulisha watu kwamba tunaishi katika kipindi ambacho Biblia inakiita “siku za mwisho” na kwamba hivi karibuni Mungu ‘atafanya vitu vyote kuwa vipya.’ (2 Timotheo 3:1) Tunakutia moyo uchunguze Biblia na ujifunze kuhusu tumaini zuri unaloweza kuwa nalo. Pia tunakusihi ukubali mwaliko huu: “Mtafuteni Yehova, wakati anapoweza kupatikana. Mwiteni akiwa bado yupo karibu.” (Isaya 55:6) Badala ya kuongozwa na majaliwa, unaweza kujichagulia jinsi maisha na wakati wako ujao utakavyokuwa!

[Blabu katika ukurasa wa 8]

“Tazama! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya”