Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mtu Mwenye Unyenyekevu na Ujasiri

Mtu Mwenye Unyenyekevu na Ujasiri

Kwa Ajili ya Vijana

Mtu Mwenye Unyenyekevu na Ujasiri

Yona—Sehemu ya 1

Maagizo: Fanya zoezi hili katika mazingira matulivu. Unaposoma maandiko, jiwazie ukiwa katika matukio yanayozungumziwa. Wazia kikao. Sikia sauti. Hisi kama wahusika wakuu wanavyohisi. Wazia kwamba masimulizi haya ni halisi kabisa.

1 CHUNGUZA TUKIO HILI.—SOMA YONA 1:1-17; 2:10–3:5.

Unaweza kuwazia dhoruba hiyo na jinsi upepo unavyovuma?

․․․․․

Unatambua hisia gani katika sauti ya Yona na ya mabaharia walio katika meli?

․․․․․

Eleza mambo ambayo huenda Yona alikuwa akifikiria alipokuwa akizama baharini na baada ya kumezwa na samaki mkubwa. (Soma Yona 2:1-9.)

․․․․․

2 CHIMBA ZAIDI.

Ni watu wa aina gani walioishi Ninawi, na kwa nini huenda mwanzoni Yona alisita kuzungumza nao? (Nahumu 3:1)

․․․․․

Unafikiri Ninawi lilikuwa “jiji kubwa kwa Mungu” kwa njia gani? (Yona 3:3; 2 Petro 3:9)

․․․․․

Kwa kutaja mambo waziwazi anapozungumza kuhusu kosa lake na kumhusu Mungu, Yona anafunua nini kujihusu? (Soma tena Yona 1:9, 10.)

․․․․․

Huenda Yona alijua jinsi gani yaliyotukia katika meli baada ya yeye kutupwa baharini? (Soma tena Yona 1:15, 16.)

․․․․․

3 TUMIA MAMBO ULIYOJIFUNZA. ANDIKA MAMBO ULIYOJIFUNZA KUHUSU . . .

Woga.

․․․․․

Unyenyekevu.

․․․․․

Ujasiri.

․․․․․

Maoni ya Yehova kuwahusu watu, hata wale ambao huenda wakaonekana kuwa waovu.

․․․․․

4 NI MAMBO GANI KATIKA SIMULIZI HILI AMBAYO YAMEKUGUSA MOYO SANA, NA KWA NINI?

․․․․․

Ili kufanya utafiti zaidi, ona gazeti la Mnara wa Mlinzi la Januari 1, 2009, ukurasa wa 25-28.

SOMA HABARI ZAIDI ZA BIBLIA, KWENYE INTANETI www.watchtower.org