Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Amani na Usalama wa Kweli—Utapatikana Lini?

Amani na Usalama wa Kweli—Utapatikana Lini?

Hotuba ya Pekee

Amani na Usalama wa Kweli—Utapatikana Lini?

Kwa maelfu ya miaka, wanadamu wametafuta amani na usalama. Lakini wameshindwa kupata amani ya kweli. Kwa nini? Biblia inatoa sababu mbili za msingi zinazofanya iwe vigumu kupata amani. Pia inatoa uhakikisho huu unaochangamsha moyo: Mungu ameahidi kwamba wanadamu watafurahia amani na usalama wa kweli na wa kudumu duniani kote.

Amani na usalama huo utapatikana jinsi gani na wakati gani? Unahitaji kufanya nini ili ufurahie hali hizo nzuri? Maswali hayo yatajibiwa kwenye hotuba ya pekee “Amani na Usalama wa Kweli—Utapatikana Lini?” Hotuba hiyo inayotegemea Biblia itatolewa duniani kote katika nchi zaidi ya 230. Katika sehemu nyingi, hotuba hiyo itatolewa kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova siku ya Jumapili, Aprili 18, 2010. Mashahidi katika eneo lenu watafurahi kuwaambia mahali na wakati ambapo hotuba hiyo itatolewa. Unakaribishwa kwa uchangamfu uhudhurie.