Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Yesu “Huondolea Mbali Dhambi ya Ulimwengu”

Yesu “Huondolea Mbali Dhambi ya Ulimwengu”

Yesu “Huondolea Mbali Dhambi ya Ulimwengu”

Yohana Mbatizaji alisema kwamba Yesu “huondolea mbali dhambi ya ulimwengu.” (Yohana 1:29) Hilo linarejelea daraka la Yesu la kukomboa wanadamu watiifu.

Lakini, kwa nini ilikuwa lazima Yesu afe ili awaokoe watenda-dhambi?

Alitimiza nini kwa kutoa uhai wake kwa hiari?

Ni nani wanaofaidika na kifo chake?

Kifo chake kina umuhimu gani kwako?

Kila mwaka, Mashahidi wa Yehova hukusanyika ili kuadhimisha Ukumbusho wa kifo cha Yesu. Mwaka huu, Ukumbusho huo utafanywa Jumapili (Siku ya Yenga), Aprili (Mwezi wa 4), tarehe 17, baada ya jua kutua.

Mashahidi wa Yehova wanakualika kwa uchangamfu ujiunge nao katika kuchunguza umuhimu wa kifo cha Yesu. Maswali yaliyo hapo juu yatajibiwa kwa kutumia Biblia.

Unaweza kuhudhuria kwenye Jumba la Ufalme lililo karibu. Waulize Mashahidi wa Yehova walio karibu nawe kuhusu saa hususa na mahali pa kukutania.