Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa Yenye Furaha

Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa Yenye Furaha

Jifunze Kutoka Katika Neno la Mungu

Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa Yenye Furaha

Makala hii inazungumzia maswali ambayo huenda umejiuliza na inakuonyesha mahali unapoweza kupata majibu katika Biblia yako. Mashahidi wa Yehova watafurahi kuzungumzia majibu hayo pamoja nawe.

1. Kwa nini ni muhimu kufunga ndoa ili familia iwe yenye furaha?

Yehova, Mungu mwenye furaha, ndiye aliyeanzisha mpango wa ndoa. Ndoa ni muhimu ili familia iwe yenye furaha kwa sababu mume au mke anakuwa na mwenzi wa kushirikiana naye, nao watoto wanalelewa katika mazingira salama. Mungu ana maoni gani kuhusu ndoa? Anataka ndoa iwe mpango wa kudumu, muungano ulioandikishwa kisheria kati ya mume na mke. (Luka 2:1-5) Mungu anataka waume na wake wawe waaminifu kwa mmoja na mwenzake. (Waebrania 13:4) Yehova anawaruhusu Wakristo kutalikiana na kufunga ndoa tena ikiwa tu mmoja wao amefanya uzinzi.—Soma Mathayo 19:3-6, 9.

2. Mume na mke wanapaswa kutendeana jinsi gani?

Yehova aliwaumba wanaume na wanawake ili wakamilishane katika ndoa. (Mwanzo 2:18) Akiwa kichwa cha familia, mume anapaswa kuandalia familia yake mahitaji ya kimwili na kuifundisha kumhusu Mungu. Anapaswa kumpenda mke wake bila ubinafsi. Waume na wake wanapaswa kupendana na kuheshimiana. Kwa kuwa waume na wake hawajakamilika, ni muhimu kujifunza kusameheana ili ndoa iwe yenye furaha.—Soma Waefeso 4:31, 32; 5:22-25, 33; 1 Petro 3:7.

3. Je, unapaswa kumwacha mume au mke wako kwa sababu tu ndoa yenu haina furaha?

Ikiwa wewe na mwenzi wako wa ndoa mna matatizo, jitahidini kutendeana kwa upendo. (1 Wakorintho 13:4, 5) Neno la Mungu halipendekezi kutengana kama njia ya kusuluhisha matatizo ya ndoa. Hata hivyo, hali inapokuwa mbaya sana, Mkristo anapaswa kuamua kama inafaa kutengana na mwenzi wake au haifai.—Soma 1 Wakorintho 7:10-13.

4. Watoto, Mungu anataka muwe na maisha ya aina gani?

Yehova anataka muwe wenye furaha. Anawapa mashauri bora kuhusu jinsi mnavyoweza kufurahia ujana wenu. Anataka mnufaike na hekima na uzoefu wa wazazi wenu. (Wakolosai 3:20) Yehova anathamini chochote mnachofanya ili kumsifu.—Soma Mhubiri 11:9–12:1; Mathayo 19:13-15; 21:15, 16.

5. Wazazi, watoto wenu wanahitaji nini ili wawe wenye furaha?

Mnapaswa kufanya kazi kwa bidii ili kuwaandalia watoto wenu chakula, makao, na mavazi. (1 Timotheo 5:8) Lakini ili watoto wenu wawe wenye furaha, mnahitaji pia kuwafundisha wampende Mungu na kujifunza kutoka kwake. (Waefeso 6:4) Upendo wenu kwa Mungu unaweza kuwagusa moyo sana watoto wenu. Mnapowafundisha watoto wenu kwa kutegemea Neno la Mungu, jambo hilo linaweza kuwasaidia wawe na maoni yanayofaa.—Soma Kumbukumbu la Torati 6:4-7; Methali 22:6.

Watoto wananufaika mnapowatia moyo na kuwapongeza. Wanahitaji pia kurekebishwa na kutiwa nidhamu. Mambo hayo yanawasaidia kuepuka mwenendo unaoweza kuwakosesha furaha. (Methali 22:15) Hata hivyo, nidhamu haipaswi kamwe kutolewa kwa ukali au kwa ukatili.—Soma Wakolosai 3:21.

Mashahidi wa Yehova wanachapisha vitabu kadhaa vinavyokusudiwa hasa kuwasaidia wazazi na watoto. Vitabu hivyo vinategemea Biblia.—Soma Zaburi 19:7, 11.

Kwa habari zaidi, ona sura ya 14 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.