Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kwa Ajili ya Vijana

Jilinde Dhidi ya Roho Waovu!

Jilinde Dhidi ya Roho Waovu!

Maagizo: Fanya zoezi hili katika mazingira matulivu. Unaposoma maandiko, jiwazie ukiwa katika matukio yanayozungumziwa. Wazia kikao. Sikia sauti. Hisi kama wahusika wakuu wanavyohisi. Wazia kwamba masimulizi haya ni halisi kabisa.

1 CHUNGUZA MATUKIO HAYA.—SOMA MWANZO 6:1-6 NA MATENDO 19:11-20.

Eleza jinsi Wanefili wanavyoonekana kama unavyowazia.

․․․․․

Unafikiri wale wanaume walihisije waliposhambuliwa na roho mwovu kama inavyoelezwa kwenye Matendo 19:13-16?

․․․․․

2 CHIMBA ZAIDI.

Ukitumia vifaa vya kufanyia utafiti unavyoweza kupata, chunguza habari zaidi kuwahusu Wanefili. Unafikiri ni kwa nini walikuwa na mtazamo huo wa kijeuri?

․․․․․

Kwa nini inaweza kusemwa kwamba roho waovu ‘waliyaacha makao yao wenyewe yanayofaa’? (Soma Yuda 6.) Kwa nini unafikiri lilikuwa jambo lisilo la asili, hata lililopotoka, kwa malaika hao kujitafutia wake wa kibinadamu?

․․․․․

Masimulizi hayo mawili ambayo umesoma yanakufundisha nini kuhusu jinsi roho waovu wanavyopendezwa sana na ngono na jeuri?

․․․․․

3 TUMIA MAMBO ULIYOJIFUNZA. ANDIKA MAMBO ULIYOJIFUNZA KUHUSU . . .

Ukatili na mtazamo wa ubinafsi wa roho waovu.

․․․․․

NJIA NYINGINE UNAZOWEZA KUTUMIA MAMBO HAYO.

Kwa kuwa roho waovu hawawezi tena kujivika miili ya kibinadamu, wanaweza kutumia njia gani zisizo za moja kwa moja ili kujaribu kukushawishi?

․․․․․

Leo, ni aina gani ya vitumbuizo ambavyo vinaonyesha mtazamo na mapendezi ya roho waovu?

․․․․․

Unaweza kuonyeshaje kwamba umeazimia kupinga uvutano wa roho waovu? (Soma tena Matendo 19:18, 19.)

․․․․․

4 NI MAMBO GANI KATIKA MASIMULIZI HAYA AMBAYO YAMEKUGUSA MOYO SANA, NA KWA NINI?

․․․․․

Ikiwa huna Biblia, waombe Mashahidi wa Yehova wakupe moja, au uisome katika Intaneti kwenye www.watchtower.org/sw