Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Vita vya Har–Magedoni Vitapiganwa Wakati Gani?

Vita vya Har–Magedoni Vitapiganwa Wakati Gani?

Vita vya Har–Magedoni Vitapiganwa Wakati Gani?

“Nikaona, na, tazama! umati mkubwa, ambao hakuna mtu aliyeweza kuuhesabu, kutoka mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na lugha . . . wa[ki]toka katika ile dhiki kuu.”​—UFUNUO 7:9, 14.

VITA vya Har–Magedoni viko karibu kupiganwa. Kwa nini tuseme hivyo?

Tayari kuna kikundi cha watu duniani pote ambao wanamtumikia Yehova na wanaishi kulingana na viwango vya juu vya Biblia. Kwa msaada wa Mungu, mamilioni ya watu kutoka mataifa yote, makabila, na lugha wanakusanyika na kufanyiza undugu wenye muungano na upendo. Mashahidi wa Yehova ndio wanaofanyiza undugu huo.​—Yohana 13:35.

Hivi karibuni Shetani atakusanya majeshi yake na kuwashambulia vikali zaidi watu hao wenye amani na ambao huenda ikaonekana ni kana kwamba hawana ulinzi. (Ezekieli 38:8-12; Ufunuo 16:13, 14, 16) Unawezaje kuwa na hakika kuhusu jambo hilo? Biblia inataja matukio hususa ambayo yanaweza kutusaidia kujua wakati ambao vita vya Har–Magedoni vitaanza. Matukio mengi yanayotajwa yanaendelea kutimia sasa.

Matukio Unayoona Yakitimia

Wanafunzi wa Yesu walimuuliza jinsi ambavyo watu wangejua kwamba “umalizio wa mfumo wa mambo” umeanza. (Mathayo 24:3) Yesu alijibu kwa kutabiri kuhusu wakati ambapo “taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme, kutakuwa na upungufu wa chakula na matetemeko ya nchi mahali pamoja baada ya pengine.” Kisha akasema: “Mambo yote hayo ni mwanzo wa maumivu ya taabu.” (Mathayo 24:7, 8) Mtume Paulo alizungumza kuhusu kipindi hichohicho na kukiita “siku za mwisho,” na akasema kwamba siku hizo zingekuwa “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.” (2 Timotheo 3:1) Kulingana na maoni yako, je, unabii huo unazungumzia matukio tunayoona leo?

Kwa nini kipindi hicho kingekuwa kigumu sana? Mtume Yohana anaeleza sababu. Alitabiri kwamba kungekuwa na “kipindi kifupi cha wakati” ambacho Shetani na roho wake waovu wangetupwa duniani. Shetani anatajwa kuwa na “hasira kali” wakati wa kipindi hicho. (Ufunuo 12:7-12) Je, unaona kwamba watu wanatenda kwa hasira na jeuri, si katika eneo fulani tu bali duniani kote?

Pia, Yesu alisema kwamba katika kipindi hicho kigumu sana, kuna kazi ya pekee ambayo ingetimizwa. Alisema hivi: “Hii habari njema ya ufalme [wa Mungu] itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mathayo 24:14) Leo, katika nchi zaidi ya 235, Mashahidi wa Yehova wanahubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu katika lugha zaidi ya 500. Magazeti mawili yanayotegemea Biblia ambayo wanachapisha, yaani, Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, ndiyo magazeti yanayosambazwa zaidi duniani kote. Pia, Mashahidi wametafsiri Biblia katika lugha 100 hivi. Kazi yao inafanywa na wajitoleaji na inategemezwa kwa michango ya hiari. Je, kampeni hii ya pekee ya kuhubiri inaweza kuwa ni utimizo wa unabii wa Yesu?

Biblia pia inataja matukio yatakayotokea kabla ya vita kati ya Yehova Mungu na wapinzani wake. Fikiria matukio matatu yaliyotabiriwa utakayoona yakitimia.

Matukio Ambayo Utaona Yakitimia Hivi Karibuni

Unabii wa 1. Biblia inasema kwamba mataifa yatatoa tangazo la kipekee la “amani na usalama.” Huenda watafikiri kwamba wanakaribia kutatua matatizo makubwa duniani. Hata hivyo, matukio yatakayofuata baada ya tangazo hilo hayatakuwa ya amani.​—1 Wathesalonike 5:1-3.

Unabii wa 2. Kisha, mataifa mbalimbali yataamua kushambulia mashirika ya kidini ulimwenguni. Katika Biblia, serikali hizo zinafananishwa na mnyama mwitu; nazo dini za uwongo za ulimwengu zinafananishwa na mwanamke aliyepanda juu ya mgongo wa huyo mnyama mwitu. (Ufunuo 17:3, 15-18) Bila kujua, mnyama mwitu huyo wa mfano atafanya mambo yote ambayo Mungu anataka afanye kwa kuharibu dini zinazodai kwa uwongo kuwa zinamwakilisha Mungu.

Kwa kutumia mifano, mtume Yohana anaelezea hali hiyo hivi: “Zile pembe kumi ulizoona, na yule mnyama-mwitu, hawa watamchukia yule kahaba na kumfanya kuwa ukiwa na uchi, nao watakula sehemu zake zenye nyama na kumteketeza kabisa kwa moto. Kwa maana Mungu alitia hilo ndani ya mioyo yao ili kutekeleza wazo lake.”​—Ufunuo 17:16, 17.

Unabii wa 3. Baada ya shambulizi hilo dhidi ya dini za uwongo kufaulu, Shetani atayachochea mataifa yawashambulie waabudu wa Yehova Mungu.​—Ufunuo 7:14; Mathayo 24:21.

Unahusikaje?

Ikiwa hujapata nafasi ya kujifunza Biblia kwa undani, inaweza kuwa vigumu kwako kuamini kwamba matukio ambayo yametajwa yatatokea. Lakini kuna sababu nzuri ya kuamini mambo yote hayo yatatimia na kwamba matukio hayo yatatokea hivi karibuni. Unabii mwingi ulio katika Biblia ambao tayari umetimia unatupa uhakikisho huo. *

Tunakutia moyo utenge wakati ili uchunguze kwa nini Mashahidi wa Yehova wanaamini kwamba “vita vya ile siku kuu ya Mungu Mweza-Yote” vimekaribia na kwa nini hupaswi kuviogopa. Waombe mzungumzie mambo ambayo Biblia inasema ni lazima ufanye ili uwe kati ya watu ambao watalindwa na Yehova Mungu. (Ufunuo 16:14) Mambo utakayojifunza yanaweza kubadili maoni yako kuhusu wakati ujao.

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 17 Ili upate uthibitisho wa kwamba unabii wa Biblia umetimia, ona sura ya 2 na sura ya 9 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

[Blabu katika ukurasa wa 8]

Je, kazi inayofanywa na Mashahidi wa Yehova inaweza kuwa ni utimizo wa unabii wa Biblia?