Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Biblia Ina Manufaa Hata Leo

Biblia Ina Manufaa Hata Leo

Biblia Ina Manufaa Hata Leo

“Neno lako ni taa ya mguu wangu, na nuru kwa barabara yangu.”​—ZABURI 119:105.

BIBLIA INATOFAUTIANAJE NA VITABU VINGINE? Vitabu vingine vinaweza kuonekana kwamba vimeandikwa kwa ustadi, lakini havifai kutoa mwongozo maishani. Pia, vitabu vya kisasa vya kutoa maelekezo vinahitaji kufanyiwa marekebisho mara kwa mara. Kwa upande mwingine, Biblia inadai kwamba “mambo yote yaliyoandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha sisi.”​—Waroma 15:4.

MFANO: Ingawa haikuandikwa kwa kusudi la kutoa mwongozo wa kitiba, Biblia ina mapendekezo yanayofaa kuhusu jinsi ya kuwa na afya nzuri na hisia zinazofaa. Kwa mfano, inasema kwamba “moyo mtulivu ni uzima wa mwili wenye nyama.” (Methali 14:30) Biblia pia inaonya hivi: “Mtu anayejitenga na wengine atatafuta mapendezi yake mwenyewe; atashindana na hekima yote inayotumika.” (Methali 18:1) Vilevile, inasema kwamba “kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”​—Matendo 20:35.

MAMBO AMBAYO UTAFITI UMEFUNUA: Utulivu, urafiki mzuri, na ukarimu unaweza kuboresha afya yako. Gazeti The Journal of the American Medical Association linasema hivi: “Wanaume wanaopandwa na hasira haraka wako katika hatari mara mbili zaidi ya kupatwa na ugonjwa wa kupooza kuliko wanaume wanaoweza kudhibiti hasira yao.” Utafiti uliofanywa kwa miaka kumi nchini Australia ulionyesha kwamba wazee ambao “wana marafiki wa karibu na pia watu wanaowaeleza mambo yao ya siri,” wanaweza kuishi kwa muda mrefu zaidi. Na katika mwaka wa 2008, watafiti nchini Kanada na Marekani waligundua kwamba “kutumia pesa kuwasaidia wengine hufanya mtu awe na furaha zaidi kuliko kutumia pesa kujinufaisha mwenyewe.”

UNA MAONI GANI? Je, unaweza kutumaini ushauri wa kitiba kutoka katika kitabu kilichoandikwa karibu miaka 2,000 iliyopita? Au je, Biblia ni kitabu cha kipekee?

[Blabu katika ukurasa wa 8

“Ninavutiwa sana na Biblia . . . kwa sababu ina ushauri mzuri wa kitiba.”​—HOWARD KELLY, M.D., MMOJA WA WAANZILISHI WA KITENGO CHA KITIBA KATIKA CHUO KIKUU CHA THE JOHNS HOPKINS