Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kwa Ajili Ya Vijana

Mungu Anayechukia Ukosefu wa Haki

Mungu Anayechukia Ukosefu wa Haki

Maagizo: Fanya zoezi hili katika mazingira matulivu. Unaposoma maandiko, jiwazie ukiwa katika matukio yanayozungumziwa. Wazia kikao. Sikia sauti. Hisi kama wahusika wakuu wanavyohisi. Wazia kwamba masimulizi haya ni halisi kabisa.

Wahusika wakuu: Ahabu, Yezebeli, Nabothi, na Eliya

Muhtasari: Akichochewa na Yezebeli , Mfalme Ahabu anaua ili kujipatia shamba la mizabibu.

1 CHUNGUZA TUKIO HILI.​—⁠SOMA 1 WAFALME 21:​1-26.

Unawazia wahusika hao wakuu walikuwa watu wa namna gani?

Ahabu ․․․․․

Yezebeli ․․․․․

Nabothi ․․․․․

Eliya ․․․․․

Unaposoma mistari ya 5-7 unafikiri sauti za Yezebeli na Ahabu zilikuwaje?

․․․․․

Unaposoma mstari wa 13, eleza jinsi unavyowazia ghasia iliyozuka.

․․․․․

Unagundua hisia gani katika sauti za Eliya na Ahabu unaposoma majibizano yao kwenye mistari ya 20-26?

․․․․․

2 CHIMBA ZAIDI.

Yezebeli anaonyesha tabia gani katika mistari ya 7 na 25?

․․․․․

Ahabu anaonyesha tabia gani katika mstari wa 4?

․․․․․

Ili afanikiwe kujipatia shamba la mizabibu la Nabothi, ni nani wengine ambao Ahabu alipaswa kuua? (Soma 2 Wafalme 9:​24-26.)

․․․․․

Yehova alimwonaje Ahabu? (Soma tena mistari ya  25 na 26. Pia, soma 1 Wafalme 16:​30-33.)

․․․․․

3 TUMIA MAMBO ULIYOJIFUNZA. ANDIKA MAMBO ULIYOJIFUNZA KUHUSU . . .

Jinsi Yehova anavyoona matendo ya ukosefu wa haki.

․․․․․

Jinsi Yehova anavyowahangaikia wale ambao wametendewa isivyo haki.

․․․․․

Jinsi Yehova alivyoonyesha kwamba yeye ni Mungu wa haki. (Soma Kumbukumbu la Torati 32:4.)

․․․․․

4 NJIA NYINGINE UNAZOWEZA KUTUMIA HABARI HIYO.

Leo, watu fulani wanawezaje kuonyesha roho kama ya Yezebeli? (Soma Ufunuo 2:​18-21.)

․․․․․

Ni katika hali gani unahitaji kuonyesha ujasiri kama wa Eliya?

․․․․․

Unapokabili matendo ya ukosefu wa haki, unaweza kuwa na uhakika gani?

․․․․․

5 NI MAMBO GANI KATIKA SIMULIZI HILI AMBAYO YAMEKUGUSA MOYO SANA, NA KWA NINI?

․․․․․

Mapendekezo Simulia simulizi hilo kama taarifa ya habari. Ripoti tukio hilo, na uwahoji wahusika wakuu wa kuwaziwa na pia mashahidi.

Tembelea www.pr418.com

Soma Biblia Kwenye Intaneti

Pakua au Chapisha Makala hii