Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Jifunze Kutoka Katika Neno La Mungu

Yesu Aliwekwa Lini Kuwa Mfalme?

Yesu Aliwekwa Lini Kuwa Mfalme?

Makala hii inazungumzia maswali ambayo huenda umejiuliza na inakuonyesha mahali unapoweza kupata majibu katika Biblia yako. Mashahidi wa Yehova watafurahi kuzungumzia majibu hayo pamoja nawe.

1. Yesu aliahidiwa ufalme gani?

Mungu aliahidi kwamba mzao wa Mfalme Daudi angetawala katika kiti cha enzi cha Mungu mpaka wakati usio na kipimo. Mzao huyo aliyeahidiwa ni Yesu, na sasa huko mbinguni anatawala akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu.​—Soma Zaburi 89:4; Luka 1:32, 33.

Daudi alipokuwa bado mvulana, Mungu alimchagua awe mfalme juu ya Waisraeli, watu wa Yehova. Daudi alipokufa, Solomoni, ambaye alichaguliwa na Yehova, aliketi kwenye “kiti cha ufalme cha Yehova.” (1 Mambo ya Nyakati 28:4, 5; 29:23) Baada ya Solomoni kufa, wafalme wengi walitawala Yerusalemu, lakini wengi wao hawakuwa waaminifu. Mwishowe, Yehova aliruhusu majeshi ya Babiloni yaharibu Yerusalemu na kumwondoa mfalme aliyekuwa akitawala. Hilo lilitukia mwaka wa 607 K.W.K. Tangu wakati huo, hakuna mfalme aliyetoka kwenye familia ya Daudi ambaye ametawala akiwa katika jiji halisi la Yerusalemu.​—Soma Ezekieli 21:27.

2. Ufalme wa Mungu ulikosa kuwakilishwa duniani kwa muda gani?

Muda mfupi baada ya Yerusalemu kuharibiwa, Yehova alimwambia nabii wake Danieli kwamba Mungu angemchagua mfalme ambaye angetawala kutoka mbinguni. Utawala huo ungeanza lini?​—Soma Danieli 7:13, 14.

Danieli alifasiri maono ambayo Mungu aliagiza kwamba mti mkubwa ukatwe, kama vile tu Mungu alivyokuwa ameamuru ufalme uliokuwa Yerusalemu ukatwe na kuharibiwa. Lakini mizizi ya mti huo haingeng’olewa ili baada ya “nyakati saba” mti huo ukue tena. Biblia inaonyesha kwamba “nyakati” tatu na nusu ni sawa na siku 1,260, hivyo “nyakati saba” ni sawa na siku 2,520. (Ufunuo 12:6, 14) Katika unabii wa Biblia, mara nyingi siku huwakilisha miaka. (Hesabu 14:34) Hivyo, Ufalme wa Mungu haungekuwepo duniani kwa miaka 2,520.​—Soma Danieli 4:10-17.

3. Yesu alianza lini kutawala akiwa Mfalme?

Mungu alimtawaza Yesu kuwa Mfalme mbinguni mwaka wa 1914, miaka 2,520 kamili baada ya Yerusalemu kuharibiwa. Hatua ya kwanza ambayo Yesu alichukua akiwa Mfalme ni kumfukuza Shetani na roho wake waovu kutoka mbinguni. (Ufunuo 12:7-10) Tukio hilo halikuonekana kwa macho ya wanadamu, lakini matokeo yake yalikuwa msukosuko ambao ulionekana. (Ufunuo 12:12) Mambo ambayo yamekuwa yakitukia tangu 1914 yanathibitisha kwamba huo ndio mwaka ambao Yesu alitawazwa kuwa Mfalme.​—Soma Mathayo 24:14; Luka 21:10, 11, 31.

4. Utawala wa Yesu unakuhusuje?

Utimizo wa unabii kuhusu utawala wa Yesu unathibitisha kwamba unaweza kutegemea Neno la Mungu. Hivi karibuni, Yesu atatumia mamlaka yake akiwa mfalme kuwaondolea wanadamu mateso yote.​—Soma Zaburi 72:8, 12, 13; Danieli 2:44.

Kwa habari zaidi ona ukurasa wa 215-218 wa kitabu hiki, Biblia Inafundisha Ninii Hasa?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

[Chati katika ukurasa wa 16, 17]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

Oktoba Oktoba

607 K.W.K.. 1914 W.K.

← Miaka 2,520 →

1000 K.W.K. 1 K.W.K. 1 W.K. 1000 W.K. 2000 W.K.

← Miaka 606.25 →← Miaka 1,913.75 →

Kuharibiwa kwa Tumia kifaa cha Mungu amfanya Yesu

ufalme uliokuwa kufanya hesabu: kuwa Mfalme mwenye

Yerusalemu 606.25 mamlaka juu

+ 1,913.75 ya mataifa

= 2,520