Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kwa Wasomaji Wetu

Kwa Wasomaji Wetu

Gazeti unalosoma sasa lilianza kuchapishwa Julai 1879. Tangu wakati huo mambo yamebadilika—na ndivyo ilivyo kwa gazeti hili. (Ona picha zilizo juu.) Kuanzia toleo hili, utaona mabadiliko zaidi yamefanywa kwenye muundo wa gazeti la Mnara wa Mlinzi. Kutakuwa na mabadiliko gani?

Katika nchi nyingi, watu wengi sana hupata habari kupitia Intaneti na wanapenda kutumia njia hiyo. Kwa kutumia kompyuta, wanaweza kupata habari zinazopatikana tu kwenye Intaneti. Vitabu vingi, magazeti ya habari, na magazeti mengineyo yanaweza kusomwa kwenye Intaneti.

Kwa sababu hiyo, hivi karibuni tumeboresha Tovuti yetu ya www.pr418.com, ili iwe yenye kuvutia zaidi na rahisi kutumia. Wale wanaotembelea Tovuti hiyo wanaweza kusoma machapisho yanayopatikana katika lugha zaidi ya 430. Hata hivyo, kuanzia mwezi huu, wale wanaotembelea Tovuti yetu wanaweza kusoma pia makala zilizoteuliwa ambazo zilikuwa zikichapishwa kwa ukawaida kwenye magazeti yetu na ambazo kwa sasa zitapatikana tu kwenye Tovuti hiyo. *

Kwa kuwa makala nyingi zitapatikana tu kwenye Intaneti, toleo la watu wote la gazeti la Mnara wa Mlinzi litapunguzwa kutoka kurasa 32 hadi 16, kuanzia toleo hili. Tayari gazeti la Mnara wa Mlinzi linatafsiriwa katika lugha 204. Kwa kuwa litapunguzwa kurasa, huenda sasa ikawezekana kulitafsiri katika lugha nyingi zaidi.

Ni matumaini yetu kwamba mabadiliko hayo yatatuwezesha kuwafikia watu wengi zaidi na ujumbe wa Biblia unaookoa uhai. Tumeazimia kuendelea kutoa habari nyingi zenye kuelimisha na zinazovutia—zinazochapishwa na pia zinazopatikana kwenye Intaneti—ili kuwafaidi wasomaji wetu wengi wanaoiheshimu Biblia na wanaotaka kujua inafundisha nini hasa.

Wachapishaji

^ fu. 5 Baadhi ya makala zitakazopatikana tu kwenye Intaneti ni: “Kwa Ajili ya Vijana,” ambazo zitakuwa na mazoezi ya Biblia kwa ajili ya vijana, na “Masomo Yangu ya Biblia,” mfululizo ulioandaliwa kwa ajili ya wazazi kutumia pamoja na watoto wenye umri usiozidi miaka mitatu.