Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Jinsi Mungu Anavyowajali Viziwi

Jinsi Mungu Anavyowajali Viziwi

 Kuna viziwi milioni 70 hivi ulimwenguni pote, wengi wao hutumia moja ya zaidi ya lugha 200 za ishara ili kuwasiliana. Kwa kusikitisha, mara nyingi viziwi hutendewa isivyo haki na watu wengi kama ripoti zifuatazo zinavyoonyesha:

  •   “Ulimwenguni pote, haki za viziwi na za watu wenye matatizo ya kusikia zinapuuzwa.”​—Shirika la Kitaifa la Viziwi (Marekani).

  •   “Viziwi katika nchi zinazoendelea ndio watu maskini zaidi, na ni vigumu kwao kupata elimu wanayohitaji, ajira, na hata habari.”​—Shirikisho la Viziwi Ulimwenguni.

 Mungu anahisije kuhusu viziwi? Biblia inasema nini kuwahusu? Mashahidi wa Yehova wanafanya nini leo ili kuwasaidia?

Mungu Anawaonaje Viziwi?

 Biblia inafunua kwamba Yehova a Mungu anawajali viziwi. Anataka watendewe kwa haki na pia wanufaike na elimu anayotoa.

 Andiko: “Usimtukane kiziwi.”​—Mambo ya Walawi 19:14.

 Maana: Sheria ambayo Yehova aliwapa Waisraeli wa kale ililinda haki za viziwi.

 Andiko: “Mungu hana ubaguzi.”​—Matendo 10:34.

 Maana: Yehova anawajali watu wa namna zote bila kuangalia utamaduni, malezi, na lugha yao, kutia ndani viziwi.

 Andiko: “Yesu akaondoka ili kutembelea majiji na vijiji vyote, . . .  na kuhubiri habari njema ya Ufalme.”​—Mathayo 9:35.

 Maana: Yesu alikuja duniani ili kuwaelimisha watu kuhusu Ufalme wa Mungu na kile ambao Ufalme huo utawafanyia wanadamu—kutia ndani viziwi.​—Mathayo 6:10.

 Andiko: Yesu hata alifanya “viziwi wasikie na wasio na uwezo wa kusema, wazungumze.”​—Marko 7:37.

 Maana: Yesu alionyesha mambo ambayo Ufalme wa Mungu utatimiza wakati ambapo viziwi wataweza kusikia na kuzungumza. Katika pindi hii, Yesu alitumia ishara kuwasiliana na kiziwi kabla ya kumrudishia uwezo wa kusikia na kuzungumza.​—Marko 7:31-35.

 Andiko: “Masikio ya viziwi yatazibuliwa.”​—Isaya 35:5.

 Maana: Yehova alitabiri kwamba viziwi watasikia.​—Isaya 29:18.

Jinsi Mashahidi wa Yehova Wanavyowasaidia Viziwi Leo

 Mashahidi wa Yehova huwahubiria viziwi ulimwenguni pote kuhusu ujumbe wa Mungu unaotupa tumaini. Tunafanya nini ili kutimiza kazi hiyo? Tunatokeza Biblia na video za kufundishia Biblia katika zaidi ya lugha 100 za ishara. Pia, tunafundisha Biblia na kuongoza mikutano ya Kikristo katika lugha ya ishara. Tunatoa huduma hizo zote bila malipo kwa ajili ya yeyote anayetaka msaada wa Mungu. Kwa nini? Kwa sababu Yesu alisema: “Mlipokea bure, toeni bure.”​—Mathayo 10:8.

 Unaweza kufungua habari hizi kwenye mtandao au kuzipakua kwenye kifaa chako kupitia:

 JW.ORG. Bofya alama ya kubadili lugha iliyo juu kushoto ukiwa katika tovuti hii ili kupata habari katika lugha fulani ya ishara.

 Programu ya JW Library Sign Language. Sakinisha hii programu bila malipo kwenye kifaa chako, nawe utaweza kupakua au kutazama video katika lugha ya ishara.

Ni Habari za Aina Gani Tunazoandaa Ili Kuelimisha watu?

 Biblia ya lugha ya ishara. Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika Lugha ya Ishara ya Marekani ndiyo Biblia ya kwanza kamili ya lugha ishara duniani. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya sasa inapatikana ikiwa nzima au kwa sehemu katika lugha nyingi za ishara, na zinaendelea kuongezeka kila mwaka. (Ili kuona orodha ya lugha au kusoma Biblia kupitia video zinazopatikana mtandaoni, ona sanduku  Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Biblia katika Lugha ya Ishara.”)

 Video zinazofundisha Biblia. Mashahidi wa Yehova wametokeza video za lugha ya ishara zinazowasaidia watu waelewe Biblia na waweze kutumia ushauri uliomo wakiwa . . .

 Masomo ya kujifunzia Biblia nje ya darasa. Unaweza kufundishwa ujumbe unaopatikana katika Biblia kwa kutumia lugha ya ishara na mwalimu wako binafsi bila malipo. Chunguza jinsi masomo haya yanavyoendeshwa.

 Jeson Senajonon anaishi nchini Filipino. Ona jinsi masomo haya ya kujifunzia Biblia yalivyomsaidia kusitawisha urafiki wa karibu na Mungu.

 Mario Antúnez alikuwa kasisi nchini Honduras. Ona jinsi alivyopata majibu ya maswali yake ya Biblia, kama alivyoeleza katika simulizi la maisha yake lenye kichwa “Nilikuwa na Maswali Mengi Kuliko Majibu.”

 Mikutano na matukio mengine. Tuna makutaniko na pia vikundi vya lugha ya ishara duniani pote ambapo viziwi hukutanika ili kujifunza na kumtolea Mungu ibada kila juma. Hata, kuna matukio makubwa zaidi ya kujifunza Biblia yanayofanywa kila mwaka katika lugha ya ishara. Katika mikutano yetu na matukio mengine, kuna watu wanaofanya ishara kwenye mikononi ya watu ambao ni viziwi na vipofu. Pia tunatokeza machapisho katika maandishi ya vipofu bila malipo.

 José Luis Ayala anaishi Mexico. Alizaliwa akiwa kiziwi kisha akawa kipofu. Soma jinsi alivyosaidiwa hadi akawa mwalimu mzuri wa Biblia.

a Yehova ni jina la kibinafsi la Mungu. (Zaburi 83:18) Ona makala “Yehova Ni Nani?