Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Manuel Reino Berengui/DeFodi Images via Getty Images

ENDELEA KUKESHA!

Je, Kweli Kombe la Dunia Linaweza Kuwaunganisha Watu?​—Biblia Inasema Nini?

Je, Kweli Kombe la Dunia Linaweza Kuwaunganisha Watu?​—Biblia Inasema Nini?

 Inakadiriwa kwamba watu bilioni tano watatazama michezo ya Kombe la Dunia ya FIFA inayofanywa kuanzia Novemba 20 hadi Desemba 18, 2022. Watu wengi wanahisi kwamba matukio kama hayo ya michezo yana uwezo wa kutimiza mengi kuliko kuwakutanisha mashabiki tu.

  •   “Michezo ina uwezo wa kubadili ulimwengu. Ina nguvu za kuwachochea watu. Ina nguvu za kuunganisha watu katika njia ya pekee.​—Nelson Mandela, aliyekuwa rais wa Afrika Kusini.

  •   “Mpira . . . unatuunganisha katika tumaini, unatuunganisha katika shangwe, unatuunganisha kwa kutupatia mchachawo wa kutenda, na unatuunganisha katika upendo, licha ya tofauti zetu.”​—Gianni Infantino, rais wa FIFA. a

 Je, Kombe la Dunia au tukio lolote la michezo linaweza kutimiza malengo kama hayo ya juu? Je, kuna tumaini la kupata amani na umoja?

Je, ni chanzo cha umoja?

 Kombe la dunia la mwaka huu limehusisha mambo mengi kuliko mpira. Michezo hiyo imetokeza majadiliano juu ya masuala ya kijamii na ya kisiasa yanayohusu haki za kibinadamu, ubaguzi wa rangi, na usawa wa kiuchumi.

 Hata hivyo, watu wengi huona kwamba mchezo wa kimataifa kama vile Kombe la Dunia huandaa burudani. Hata hivyo, matukio hayo hayawezi kuleta umoja wa kudumu hata ingawa watu wangependa hilo. Badala yake, mara nyingi yanatokeza mitazamo na matendo yanayosababisha migawanyiko ambayo Biblia ilisema ingekuwa ishara ya kipindi kinachoitwa “siku za mwisho.”​—2 Timotheo 3:1-5.

Tumaini la kweli la umoja ulimwenguni

 Biblia inatupa tumaini la kweli la kuleta umoja ulimwenguni. Inaahidi kwamba watu wote duniani wataunganishwa chini ya serikali ya mbinguni inayoitwa “Ufalme wa Mungu.”​—Luka 4:43; Mathayo 6:10.

 Mfalme wa Ufalme huo, Yesu Kristo, atahakikisha kutakuwa na amani ulimwenguni pote. Biblia inasema hivi:

  •   “Mwadilifu atasitawi, na amani itakuwa nyingi.”​—Zaburi 72:7.

  •   “Atamwokoa maskini anayelilia msaada . . . atawaokoa kutoka katika ukandamizaji na ukatili.”​—Zaburi 72:12, 14.

 Hata leo, tayari mafundisho ya Yesu yamewaunganisha mamilioni ya watu katika nchi 239. Wamejifunza kuacha kuwa na chuki. Ili ujifunze mengi zaidi, soma mfululizo wa makala zenye kichwa “Jinsi ya Kushinda Chuki.”

a Fédération Internationale de Football Association, shirikisho la mpira wa miguu duniani.