Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

ENDELEA KUKESHA!

Biblia Inasema Nini Kuhusu Kuabudu Sanamu?

Biblia Inasema Nini Kuhusu Kuabudu Sanamu?

 Kulingana na Shirika la Habari la Kanisa Katoliki (Catholic News Service), Papa Francis alisimama mbele ya sanamu ya Maria akiwa “amefunga macho yake na kuinamisha kichwa chake kutoa sala kimyakimya” wakati wa sherehe iliyofanywa Machi 25, 2022 kwenye kanisa la St. Peter’s Basilica. “Alimsihi Maria” alete amani. Ripoti ya Habari ya Vatican iliongezea kwamba “Papa alisali Tendo la Kuwaweka Wakfu wanadamu wote, hasa Urusi na Ukrainia, kwa Moyo Safi wa Maria.”

 Una maoni gani? Je, ni sawa kusali mbele ya sanamu au kuzitumia katika ibada? Fikiria mistari ya Biblia ifuatayo:

  •   “Usijitengenezee sanamu ya kuchongwa au mfano wa kitu chochote kilicho juu mbinguni au kilicho chini duniani au kilicho ndani ya maji chini ya dunia. Usiviinamie wala kushawishiwa kuviabudu, kwa sababu mimi, Yehova Mungu wako, ni Mungu ninayetaka watu waniabudu mimi peke yangu.”​—Kutoka 20:4, 5. a

  •   “Sanamu zao ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya mwanadamu. Zina kinywa, lakini haziwezi kuongea; zina macho, lakini haziwezi kuona; zina masikio, lakini haziwezi kusikia; zina pua, lakini haziwezi kunusa; zina mikono, lakini haziwezi kugusa; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; hazitoi sauti yoyote kwa koo zake. Watu wanaozitengeneza watakuwa kama sanamu hizo, na pia wote wanaozitumaini.”​—Zaburi 115:4-8.

  •   “Mimi ni Yehova. Hilo ndilo jina langu; sishiriki utukufu wangu na yeyote, wala kuzipa sanamu za kuchongwa sifa yangu.”​—Isaya 42:8, maelezo ya chini.

  •   “Ikimbieni ibada ya sanamu.”​—1 Wakorintho 10:14.

  •   “Jiepusheni na sanamu.”​—1 Yohana 5:21.

 Ili upate habari zaidi kuhusu kile ambacho Biblia inasema kuhusu kutumia sanamu katika ibada, soma makala “Maoni ya Biblia—Sanamu” au utazame video Je, Mungu Anakubali Sanamu Zitumiwe Katika Ibada?

 Huenda pia ukapendezwa kujua kile ambacho Biblia inasema kuhusu habari hizi:

Photo credit: Vincenzo Pinto/AFP via Getty Images

a Yehova ni jina la kibinafsi la Mungu. (Zaburi 83:18) Ona makala “Yehova Ni Nani?