Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

alashi/​DigitalVision Vectors via Getty Images

ENDELEA KUKESHA!

Kwa Nini Kuna Chuki Sana Leo?​—⁠Biblia Inasema Nini?

Kwa Nini Kuna Chuki Sana Leo?​—⁠Biblia Inasema Nini?

 Leo vyombo vya habari vimejaa habari kuhusu watu wanaosema maneno makali yanayosababishwa na chuki, wanaofanya mambo ya kikatili kwa sababu ya ubaguzi, na pia kuna habari nyingi kuhusu vita.

  •   “Kuna maneno mengi makali yenye chuki katika mitandao ya kijamii kuliko wakati mwingine wowote kwa sababu ya mgogoro unaoendelea kati ya Israel na Gaza na kwa sababu ya watu wanaochochea jeuri na chuki.”​—The New York Times, Novemba 15, 2023.

  •   “Tangu Oktoba 7, chuki na jeuri zimeongezeka ghafula kwa sababu ya ubaguzi.”​—Dennis Francis, rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Novemba 3, 2023.

 Maneno makali yenye chuki, jeuri, na vita ni mambo ambayo yamekuwapo. Biblia inataja kuhusu watu walioishi zamani ambao “[walilenga] maneno yao ya ukatili kama mishale” na ambao walifuatia vita na jeuri. (Zaburi 64:3; 120:7; 140:1) Hata hivyo, Biblia inafafanua kwa nini chuki tunayoona leo ni tofauti.

Chuki​—Ishara katika nyakati zetu

 Biblia inafunua sababu mbili zinazoonyesha kwa nini chuki imekuwa jambo la kawaida leo.

  1.  1. Ilitabiri mapema kuhusu kipindi ambacho “upendo wa wengi utapoa.” (Mathayo 24:12) Badala ya kuwa na upendo, watu wengi wangekuwa na chuki.​—2 Timotheo 3:1-5.

  2.  2. Chuki tunayoona leo ulimwenguni inatokana na uvutano wa yule mwovu Shetani Ibilisi aliye na nia mbaya. Biblia inasema kwamba “ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu.”​—1 Yohana 5:19; Ufunuo 12:9, 12.

 Hata hivyo, Biblia inafunua pia kwamba hivi karibuni, Mungu ataondoa mambo yanayosababisha chuki. Jambo lingine atakalofanya ni kuondoa madhara yote yanayosababishwa na chuki. Biblia inaahidi hivi:

  •   Mungu “atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”​—Ufunuo 21:4.