Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

ENDELEA KUKESHA!

Mashahidi wa Yehova na Yale Maangamizi Makubwa ya Wayahudi—Biblia Inasema Nini?

Mashahidi wa Yehova na Yale Maangamizi Makubwa ya Wayahudi—Biblia Inasema Nini?

 Januari 27, 2023, watu wengi wataadhimisha Siku ya Kimataifa ya Maangamizi Makubwa ya Wanazi. Huenda ukatili huo uliotukia zaidi ya miaka 75 iliyopita ukafanya ujiulize kwa nini Mungu aliruhusu mauaji hayo yatendeke.

 Wayahudi walionewa na kuteswa kikatili katika kipindi hicho. Wanazi walipanga mauaji ya mamilioni ya Wayahudi. Isitoshe, walifanya mipango ya kuwatesa na kuwaua washiriki wa vikundi vingine pia. Mashahidi wa Yehova walikuwa miongoni mwa vikundi hivyo na waliteswa kwa sababu ya imani yao inayotegemea Biblia.

“Wakati ujao na tumaini”

 Watu wengi wanahofia kwamba Maangamizi kama hayo yanaweza kutukia tena. Inapendeza kwamba Biblia inaahidi wakati ujao misiba kama hiyo haitakuwapo tena.

  •   “‘Kwa maana ninajua vizuri mawazo ninayofikiria kuwaelekea ninyi,’ asema Yehova, ‘mawazo ya amani, wala si ya msiba, ili niwape ninyi wakati ujao na tumaini.’”​—Yeremia 29:11. a

 Tumaini hilo litatimizwa Yehova Mungu atakapochukua hatua ya kukomesha uovu na kuondoa uharibifu ambao uovu umetokeza. Hivi karibuni Mungu:

  •   Ataondoa watu waovu ambao wanawadhuru wengine.​—Methali 2:22.

  •   Atawaponya wote ambao wameteseka.​—Ufunuo 21:4.

  •   Atafufua wale waliokufa ili waishi duniani.​—Yohana 5:28, 29.

 Tumaini linalopatikana katika Biblia, linategemeka kabisa. Ili ujue kwa nini linategemeka, tunakualika ujifunze Biblia ukiongozwa na mwalimu, bila malipo.

a Yehova ni jina la kibinafsi la Mungu.​—Zaburi 83:18.