Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Photo by Zhai Yujia/China News Service/VCG via Getty Images

ENDELEA KUKESHA!

Mafuriko Yanayosababisha Madhara—Biblia Inasema Nini?

Mafuriko Yanayosababisha Madhara—Biblia Inasema Nini?

 Ulimwenguni pote, watu wengi wanakabili mafuriko yanayosababisha madhara. Zifuatazo ni baadhi ya ripoti:

  •   “Katika siku chache zilizopita, mji mkuu wa China umekumbwa na mvua kubwa zaidi kumwagika katika miaka 140 iliyopita, baada ya kupata . . . milimita 744.8 za mvua kuanzia Jumamosi hadi Jumatano.”​—AP News, Agosti 2, 2023.

  •   “Alhamisi ilikuwa siku ya pili ambayo Kimbunga Khanun kilitokeza mvua kubwa na upepo wenye nguvu kusini mwa Japani na kusababisha vifo vya watu wawili. . . . Dhoruba hiyo inatarajiwa kutokeza mita 0.6 za mvua katika eneo la milimani la Taiwan.”​—Shirika la Habari la Deutsche Welle, Agosti 3, 2023.

  •   “Mafuriko ya mwisho-juma [kule Nova Scotia] yalisababishwa na mvua kubwa zaidi kulikumba eneo la Atlantiki la Kanada kwa miaka 50 iliyopita.”​—Shirika la Habari la BBC, Julai 24, 2023.

 Biblia inasema nini kuhusu matukio kama hayo?

Ishara ya “siku za mwisho”

 Biblia inafunua kwamba tunaishi katika kipindi cha wakati kinachoitwa “siku za mwisho.” (2 Timotheo 3:1) Yesu alitabiri kwamba katika wakati wetu, tungejionea “mambo yenye kuogopesha,” au matukio yenye kutisha. (Luka 21:11) Mabadiliko ya hali ya hewa yamechangia kutokea kwa matukio yenye kutisha ya hali ya hewa ambayo hayawezi kutabiriwa, yanayotokea mara nyingi zaidi, na ambayo ni makubwa isivyo kawaida.

Sababu ya kuwa na tumaini

 Biblia inatuambia kwamba mambo mengi yenye kuogopesha yanayotokea duniani leo yanatupatia sababu ya kuwa na tumaini. Kwa nini? Yesu alisema hivi: “Mtakapoona mambo hayo yakitukia, jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.”​—Luka 21:31; Mathayo 24:3.

 Matukio tunayojionea yanaashiria kwamba hivi karibuni Ufalme wa Mungu utadhibiti kikamili nguvu za asili za dunia, kutia ndani mzunguko wa maji.​—Ayubu 36:27, 28; Zaburi 107:29.

 Ili ujifunze mengi kuhusu Ufalme wa Mungu utakavyorekebisha dunia, ona makala yenye kichwa “Ni Nani Atakayeiokoa Dunia?